webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

FURAHA PEKEE

Gari ya Edrian ilisimama kwenye geti la kuingia nyumbani kwao Aretha ikiwa tayari ni saa moja na nusu usiku. Kwa namna walivyoonekana hawakutamani kuachana kwa wakati huo..

Ed akajikaza na kumwambia Aretha washuke

"Aaah" Aretha aliitika

"Retha twende nisimpe mama wasi wasi" akazima gari na kufungua mlango,

"Rian" Aretha akamuita Ed ambaye aligeuka kushuka lakini akarudi mkono ukiwa umeshika kitasa cha mlango wa gari

"Aaahm" akaitika Ed huku akimuangalia Aretha katika mwanga hafifu uliopenya kwenye gari ukitokea kwenye moja ya taa iliyokuwa pale nje.

"Aaahmm..amm.."Aretha akichezea vidole vyake alipatwa kigugumizi, uso wake ulitazama chini

"Retha unataka kuniambia nini?" Ed akatoa mkono kwenye mlango akamshika Aretha mkono kitendo kilichomfanya amwangilie usoni.

Kitu kilichofuatia kikamshangaza Ed, Aretha akamsogelea kwa haraka na kumkumbatia..

"I love you Rian.."

"I love you so much Retha." Edrian akamjibu na kumkumbatia

Akatabasamu kwa furaha, maana muda wote huo ni yeye ndie alikuwa wa kwanza kwa kila hatua, sasa Aretha amemkumbatia mwenyewe.

"Retha, kesho tutaonana sawa eeh" akamwambia kwa sauti ya chini karibu na sikio lake. Aretha akamuacha na hakumwangalia Ed akashuka kwenye gari na kusimama getini huku akigonga taratibu.

Ed akafuatia nyuma yake, wakasimama wakisubiri geti lifunguliwe. Frans mdogo wake Aretha akafungua na kuwakaribisha ndani. Aretha hakugeuka kabisa nyuma akaingia ndani.

"Frans, asante kutufungulia" Ed akasema akiwa na tabasamu usoni

"Ooh hamna shida karibu bro"

Mama yake Aretha alikaa kwenye veranda ya mbele ya nyumba akamuona binti yake na namna alivyorudi akatabasamu zaidi.

"Mama shikamoo" Aretha akasalimia na kupitiliza hadi ndani uso wake ukionesha tabasamu na soni kwa wakati mmoja.

"Eeeh we Retha unakimbikimbia tu kusalimia gani huko" mama yake akalalamika

"Mamaa aaah"" sauti ya Aretha ikasikika kutokea ndani.

"Mama tumerudi salama, unaendeleaje?" Ed akamsalimia mama akiwa amesimama karibu na ngazi za kuingia pale alipoketi.

"Sawa, mwanangu hongereni naona mwenzio kachoka hataki hata kusalimia" mama akamjibu

"Hahahaha hapana mama" Ed akacheka kidogo

"Karibu ndani mwanangu" mama akinuka kumkaribisha Ed,

"Haaam hapana mama, asante sana naomba nirudi sasa. Wakati mwingine nitakuja tuongee"

"Aaaah basi sawa mwanangu" mama akamkubalia Ed ambaye alirudi kwenye gari ili kuondoka. Akamshukuru sana Frans ambaye alitoka ili kufunga geti.

Edrian akaingia kwenye gari na kuwasha kuanza safari kurudi nyumbani kwake.

"Thank you Retha, ni kama ninaanza kuishi"

Ed akajisemea.

Siku hii ilikuwa na furaha kuu mno kwa Ed, akatamani isiishe lakini asingeweza kukaa na Aretha muda wote.

Wakati akielekea barabara kuu alihisi kuona gari kama ile iliyokuwa ikimfuatilia siku chache nyuma lakini hakutaka kuiharibu siku yake ambayo ilimuacha akiogelea katika furaha ya kipekee. Aliona ni upendeleo wa ajabu kwamba yeye na Aretha wamekubaliana kwa wepesi.

Tabasamu la Ed lilikatishwa na simu iliyoita, na alipoiangalia sura yake ikawa kikazi zaidi.

Akapokea

"Hellow Captain" akaongea

"Umetoka hapo nyumbani kwao Aretha kuna gari imesimama lakini hakuna anayeshuka. Nina mashaka nayo, unaweza kurudi bro" Captain aliongea

Edrian hakusubiri maelezo zaidi akageuza gari wakati huo huo na kuanza kuingia barabara iliymrudisha kwao Aretha.

Akapiga simu yake ambayo ilipokelewa na Aretha, "Rian I am so___? Kabla ya kumaliza Ed akamkatisha

"Retha mwambie Frans asifungue geti endapo kama kuna mtu atagonga getini" Ed alitoa maelekezo kwa sauti ya kawaida ili kutomfanya Aretha ashtuke..

"Rian kuna tatiz__"

"Retha, tafadhali fanya hivyo nitakwambia kwa nini baadae" Ed akamsihi Aretha

"Sawa Rian" Aretha akakata simu kitu kilichompa uhakika Ed kuwa atakuwa ameelekea kutekeleza kile alichomuagiza.

Ed alikuwa katika mwendo ambao magari mengine barabarani ilibidi yampishe. Kwa kuwa ilikuwa jumapili, foleni haikuwa kubwa hivyo ndani ya dakika chache alikata kuingia barabara iliyoingia 'moon street'. Simu yake ikaita alikuwa Captain akaamuru ipokelewe

"Bro imeondoka sasa hivi, inakuja muelekeo wako"