webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Realistic
Not enough ratings
245 Chs

NAJISIKIA VIZURI

Edrian aliketi na Aretha kwenye baraza la juu la jengo hili la Ashanti huku wakifurahia machweo ya jua yaliyoleta rangi ya dhahabu kwenye mazingira yaliyowazunguka. Kwa Aretha ilikuwa mandhari safi iliyompa mawazo mengi ya kuchora picha zake.

"Rian..naomba siku moja nikae hapa nipate kuchora mandhari hii" Aretha akiwa amesimama karibu na mtungi mkubwa wa maua alimuomba Ed

"Unaweza kuja wakati wote, nitakupatia kadi yako ya kuingilia" Ed akamjibu akiwa amekaa kwenye kiti chake

"Unamaanisha watu wengine hawaji huku?" Aretha akauliza

"Yes, ni kwa sababu za kiusalama. Huwezi jua mtu anaweza kupatumiaje mahali hapa. Ili kulinda matukio kama kujirusha chini, ni mimi pekee nina "access" na sehemu hii. Wanaokuja kufanya usafi huja huku nikiwapo."

"Ooh....ni vizuri, usalama ni wa msingi. Na mimi unaamini sitaweza kupatumia vibaya?" Aretha alizungusha macho akiwa ametabasamu

Ed akampa ishara asogee alipokuwa, Aretha akaenda, akanyoosha mkono kumwelekea. Aretha alipompatia mkono, Ed akamvuta na kumketisha miguuni pake, akamsogelea sikioni na kumwambia kwa sauti ya chini,

"Sababu hautakuwa peke yako 'princess', I will be watching you"

Aretha aliyekuwa ameweka mikono yake usoni alitabasamu huku akiinama mbele kwa kuwa sauti ya Ed ilikuwa ikipuliza kwenye ngozi ya sikio lake na kumtekenya.

Mikono ya Ed iliyopita tumboni kwa Aretha ilimpa nafasi ya kulaza kichwa chake mgongoni kwa Aretha.

"Retha" akamuita taratibu

"Mmm" akaitika

"Bado unataka kumtafuta baba?" Akauliza Ed kwa hisia za kujali

"Aahm" Aretha akashangaa

"Tunaweza kuendelea kumtafuta Retha usi__"

"Hapana Rian...usisumbuke" Aretha akamkatisha huku akijaribu kuinuka

"Usiinuke Retha, baki hapa, najisikia vizuri ukiwa mikononi mwangu"

"Eehmm" Aretha akashtuka na kurudi kuinama kisha akaendelea

"Kama yeye hanitafuti nadhani hanihitaji"

Kama msumari wa moto hisia za huzuni zikamchoma Ed akamuinua Aretha kisha naye akainuka. Akamgeuza wapate kutazamana usoni.

"Retha, usipate huzuni kwa ajili yake. Let's be happy. Hata kama siku akija ataona kiasi gani alipoteza mtu muhimu karibu yake" akamvuta na kumkumbatia

"I am here" Ed akasema alimbusu kwenye paji lake la uso. Aretha akatabasamu na kumshukuru Ed..

"Rian...thank you. Wakati wote maneno yako yanaishi ndani yangu."

Wakakumbatiana, Ed alitamani wakati huu usiishe. Kumweka Aretha kwenye mikono yake kwake ilikuwa ni shauku tangu siku ile alipomuona.

"Rian... ninamjua mama, atakuwa ameshakaa barazani ananisubiri nadhani tuanze kuondoka" Aretha akainua uso na kumwambia Ed ambaye alikuwa akichezea nywele zake kwa nyuma...

"Aaaaahhh..sawa Retha. I only want you here" akamwachia na kuondoa chupa zao za vinywaji na kuzitupa kwenye ndoo ya uchafu iliyokuwa pembeni. Wakati huo Aretha alisimama karibu na chuma kubwa lilioweka kuzuia mtu kukaribia mwisho wa ukuta wa jengo, akaangalia mwonekano wa A-Town. Akatabasamu kwa furaha...

"Retha umesahau" Ed akageuka na kuelekea alipokuwa amesimama

Aretha akageuka kwa mshangao akijiuliza amesahau nini, "mhhhh"

"Umesahau 'princess' uliniahidi nini?" Ed akasimama karibu nae akimuangalia machoni..

"Sikumbuki Rian.." Aretha akajitahidi kukumbuka

"Picha yangu uliniahidi"

"Ooooh Rian..nisamehe" Aretha akamsogelea Ed na kumshika mikono mara alipoambiwa alisahau picha..

Ed akatabasamu akimuangalia alivyokuwa ameshika mikono yake,

"Okay, utanieletea lini?"

Aretha akatulia na kuiachia mikono ya Ed akafikiri, "Jumanne?"

"Kwa nini isiwe kesho?" Akamuuliza akiinua nyusi zake juu akitabasamu

"Aahmm" Aretha nae akamwangalia usoni akang'ata mdomo wake wa chini akifikiria asijue macho ya Ed sasa yalimwangalia mdomoni na si machoni tena..

"Haa. .haya sawa nitakuletea kesho"

"Unatoka darasani saa ngapi?" Ed akamuuliza

"Saa saba mchana"

"Utaibeba picha hadi chuoni?" Akauliza Ed

"Yes.. kuna mahali nitaiweka kabla sijatoka darasani"

Ed ambaye macho yake bado yaliangalia midomo ya Aretha "nitakuja kukuchukua chuo ukanipatie picha yangu nyumbani"

"Aahmm" Aretha akashangaa, kabla hajatoa maelezo, midomo yake ikavamiwa na ile ya Ed na busu zito likawapoteza.