webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

TAYARI KUUPINDUA ULIMWENGU

Mama akaelekea hadi kitandani kuketi na hakuacha kuona koti alilokuja nalo binti yake likiwa chini ya mito miwili iliyokuwa kitandani!

Aretha akajiwahi kukaa karibu na ile mito akijaribu kumziba mama yake asilione lile koti,

"Retha, nimeshaliona, niambie ni la nani?" Mama akamwambia huku akimtazama kwa jicho la upole...

Kwa namna Aretha alivyoshtuka mama yake akatabasamu na kunyoosha mkono wake uliolivuta koti.

"Mm..a..mama..jamani" Aretha akapata kigugumizi cha ghafla...

"Mwanangu wala usione aibu, natamani tu kumfahamu mwenye koti hili, ni la Derrick?"

"Hapana mama...sio Derrick." akamkatalia kwa haraka

"Niambie binti yangu" mama akamwambia kwa kumsihi mwanae maana alitamani kujua

Akashusha pumzi kwa nguvu kisha akaanza kumwambia, "mama hivi unafahamu Derrick ni mdogo wa Edrian Simunge?"

"Hapana sikujua kabisa, maana Derrick hakutaja jina la Simunge wakati alipojitambulisha" Mama akajibu kwa mshangao..

Aretha akamsimulia jinsi walivyofika na hadi Edrian akamrudisha..

"Retha.... unampenda Edrian?" Mama akamshtukiza binti yake...

Aretha akatikisa kichwa akikataa huku akimlalamikia "mama aaaah unataka nini?"

"Mwanangu mimi ni mama yako... nakujua... ni aidha Derrick au Edrian?"

"Aaaarghh... Mama nataka kulala.." Aretha akaamua kukimbia mahojiano na mama yake sababu alimjua hataweza kumpa nafasi kwa kuwa ni mara ya kwanza ameonesha udhaifu kwa mwanaume.. Siku zote mama yake amekuwa akimlazimisha kuwa na urafiki na watu wa jinsi zote mbili kitu ambacho Aretha hakuwa anapenda.

Mama yake alimsisitiza wakati wote kwa sababu ya changamoto ambazo Aretha alikuwa nazo alipokuwa mtoto... Aretha hakupenda sana kuchangamana na watu sababu aliwahi kuwa mhanga wa udharirishaji kutoka kwa wanafunzi shule aliyosoma. Akiwa binti mdogo alisumbuliwa sana na kigugumizi, udhaifu huu ulichukuliwa vibaya na wengine, walimdhihaki hata kumcheka kila mara alipotaka kuongea. Aretha aliamua kuwa peke yake wakati mwingi. Alighairi kuwa na marafiki japokuwa kuna watu walijitahidi kuwa karibu naye.

"Kabla hujalala niambie hili koti unalirudisha lini au amekupatia liwe lako?"

"Ma..Mama" akafungua uso wake

Mama yake akamtazama binti yake na kutabasamu..." Niambie nikuache ulale"

"Kesho mama" akajibu kwa sauti ya chini..

"Hautalipeleka, ataliijia mwenyewe. Nimemaliza" mama akainuka na kuondoka na lile koti...

"Mama aaaaah unapeleka wapi koti la.la watu" akashusha pumzi akimuangalia mama yake akiondoka chumbani na lile koti..

Akajitupia kitandani na kushusha pumzi. Mama kwa upande wake akaenda chumbani na kuliweka koti kwenye kishikio nyuma ya mlango..

"Oooh Mungu wangu...msaidie mwanangu awe kwenye mikono sahihi" akanong'ona taratibu..

Akapanda kitandani na kulala japokuwa alitamani kumjua huyu Edrian! Akaamua kumtafuta Derrick kesho tu atakapoamka...

Na ndivyo alivyofanya...

"Hellow mwanangu Derrick!"

Baada ya salamu, mama Aretha akamuuliza Derrick kuhusu Edrian...

"Na kwa nini hukuniambia kama unatoka kwa Simunge?"

Derrick akashusha pumzi akijiuliza nini kilitokea baada ya Ed kumrudisha Aretha,

"Nisamehe mama, sikupenda kutumia hili jina maana linafahamika sana..."

"Derrick hutaniongopea mwanangu eeeeh, Niambie ukweli, kwa namna ulimfahamu binti yangu. Naomba ukweli tu mwanangu" mama alimsihi kwenye simu kiasi Derrick akajisikia kujihukumu kwa kile alichofanya..

Akaanza kumsimulia hatua ya kumuona Aretha kwenye kipindi cha Tv hadi alivyomfuatilia na kwa nini alitaka aende naye kwenye sherehe...." Mama niamini haya yote tunafanya kwa sababu tunampenda kaka na pia kwa upande wangu Aretha ni mwanamke mwema kwa ajili ya Ed." Hakumwambia kuhusu Joselyn kabisa.

Mama alibaki mdomo wazi akishangazwa na jitihada za Derrick. Kitu cha ajabu zaidi Aretha kushiriki kipindi cha TV ulikuwa ni mshangao mkubwa kwake.. akahisi kuna kitu zaidi kwa Aretha ambacho anahitaji kukifahamu.

Mwanangu, unamuamini kaka yako kwa ajili ya Aretha au unaongopa?" Akauliza mama

"Mama, si tu kwa sababu ni kaka yangu bali ni mtu ninayemfahamu kuwa akisema kitu yuko tayari kuupindua ulimwengu wote akipate kile anachotaka!" Derrick akamtetea kaka yake. Ni damu moja.