webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

SIO MARAFIKI

Edrian akamwangalia Inspekta kwa hasira , "Unataka kupata nini katika hicho unachojaribu kuuliza?"

"Rian" Aretha akamshika mkono kumrudisha nyuma Ed ambaye alisimama akiangaliana na Inspekta. Yule askari aliyekuwa pembeni akapiga hatua kusogea lakini Inspekta Sunday akampa ishara arudi nyuma

Edrian akamwangalia Aretha kisha akaketi, Inspekta akaendelea kusimama huku akitabasamu

"Samahani Mr Simunge, naona unasahau taratibu za kazi yetu, ninachofanya ni sehemu ya kazi yangu. Hii ndio sababu niliuliza kama una uhuru wa kutoa maelezo ukiwa na Aretha"

"Inspekta nakuomba mara moja tu tuongee halafu utaendelea" Aretha akamwambia Inspekta kwa kumsihi

Inspekta akaitikia na kisha akampa ishara askari ambaye alisimama pembeni watoke nje.

Baada ya mlango kufungwa Aretha akaushika mkono wa Ed akamwambia

"Rian, kuna kitu hujaniambia unahitaji kuniambia?. Tafadhali toa ushirikiano kwa polisi ili tujue n_"

"Retha, ninachokisema ndivyo ilivyokuwa, sipendi maswali yasiyo na maana tu, Sunday sio mgeni kwangu ila huwa ana maswali yasiyopasa"

"Rian ulitukuta na nguo au la?" Aretha akauliza huku akimtazama usoni Ed ambaye alimtazama kisha akainua mkono wake na kumgusa shavuni Aretha

"Niliwakuta na nguo princess" Ed akamwambia kisha akashusha mkono wake huku akikunja ngumi, Aretha hakuona ngumi ile akashuka ili akamrudishe Inspekta ndani, lakini Ed akamshika mabega kumzuia alisimama

"Nitaenda Retha" akainuka na kuelekea mlangoni, akatoka na kumkuta Inspekta akiwa amekaa kwenye benchi pembeni ya mlango huku akiandika vitu kwenye kijidaftari chake.

"Mr Simunge, mimi na wewe tunajua maelezo yasiyopotosha ukweli husaidia kufikia ukweli" Inspekta Sunday akainuka mara Ed alipopiga hatua kumsogelea

Ed akasimama, wakatazama kwa muda, kwa namna ambayo usingeweza kujua ni kwa chuki au kwa amani.

"Sunday" Ed akamuita

"Inspekta Sunday my friend" Inspekta akamwambia huku akiachia tabasamu.

Edrian naye akaachia tabasamu akamshika mkono kuonesha kumkubali kuwa ni Inspekta

"Mimi na wewe sio maadui na wala sio marafiki. Ila nina ombi moja tu kwako, tafadhali urudishe ubinadamu wako ulioupoteza kambini. Fanya kazi yako kwa utu"

"Kwa sababu ni Aretha au?" Inspekta akamuuliza huku akiinua nyusi juu

"Ndio, kwa sababu ni Aretha lakini pia ni binadamu kama wengine ambao wanastahili ubinadamu wako" Edrian akaachia tabasamu

"Hahahaha unanifundisha kazi Simunge!!!, hebu tumalize maelezo au tunarudi ndani?" Inspekta akauliza huku akimpa ishara ya kurudi ndani

"Tunarudi ndani ila usinichokoze zaidi" Edrian akajibu na kufungua mlango kisha wakapiga hatua kuingia, lakini Inspekta akamwambia kwa sauti ya kunong'ona kumfanya Edrian ageuke nyuma na kutikisa kichwa

"Tutafutane uniambie ukweli ni mizani yangu imepungua au ni kweli umedakwa kwenye mapenzi?"

********

Mara alipotoka Edrian nje ili kumrudisha Inspekta, Aretha alibaki akitafakari iwapo kile alichokisikia kilikuwa ni ukweli au la.

"Au Rian ananificha ukweli!!!" Akajiuliza Aretha, akajikagua nguo zake hakuona tofauti yoyote

"Nitamuuliza nani sasa???. Kama alinikuta sina nguo oooh Mungu wangu naomba isiwe...isiwe kabisa." Akawaza Aretha huku mikono yake akiifunika usoni mwake. Akakusudia kumuuliza Derrick walau apate ukweli lakini napo pia akajikwaa

"Aaaargh nikimuuliza akanijibu ndio ina maana na yeye aliniona? Oooh haya mambo yananichosha"

"Kile Bruno alikisema mbona kama kuna mtu aliambiwa na mtu?" Akawaza Aretha

"Nina uhakika vita hivi ni matokeo ya Joselyn bila shaka. Au nimwambie Inspekta, aaaah naweza sema ni Lyn kumbe sio, lakini yeye ndio sababu ya matatizo mengi" swali moja kwenda jingine liliendelea kichwani kwa Aretha hadi mlango ulipofunguliwa wakaingia Edrian na Inspekta.

Ed akaelekea pembeni ya Aretha akaketi, "Tunaweza kuendelea inspekta" akamwambia

Inspekta akatabasamu na kumwangalia Edrian

"Kwa maelezo yako Mr Simunge unahisi ni nani anaweza kuwa amehusika na tukio hili?"

Edrian akamwangalia Aretha kisha akarudisha macho kwa Inspekta

"Joselyn Martinez Kussah" Ed akamkazia macho Inspekta ambaye aliachia tabasamu lenye utani ndani yake