webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

NOT YOUR ENEMY

"Kuna maadui gani wanakutafuta?" Akamuuliza

"Maadui? Wa wapi hao Retha" akauliza Ed ambaye sauti yake ilikuwa na mshangao mkubwa

Aretha alipoona namna Edrian alivyoshangaa akawa kama ameshikwa na kigugumizi

"Retha unawaza nini" Edrian akamuuliza baada ya kuona kimya kimetawala kidogo

"Aaaah. .naona unavyonisisitiza kuwa mwangalifu unanipa maswali Rian" Aretha akajitahidi kujieleza

"Oooh ni kawaida kukutaka uchukue tahadhari, nilikwambia tangu mwanzo kuwa nina maadui ambao wananich_" kabla ya kuendelea sauti ya mlango uliogongwa upande wa Edrian ulikatisha maongezi yaliyoendelea, alipotaka kuendelea Aretha akawahi kumwambia

"Rian tutaongea hata baadae, tafadhali endelea na majukumu yako" Aretha akamsihi

"Retha ni mimi ndio nimepiga simu hahaha" Edrian akamtania huku akimruhusu aliyegonga kuingia

"Sawa Rian lakini uko kazini" Aretha akajitetea

"Nitakupigia baadae Retha. Love you" akakata simu bila kusubiri jibu la Aretha.

Aretha akatabasamu baada ya Edrian kupata simu, "afadhali amenisikiliza"

Kabla ya kuendelea na kupanga vifaa vyake simu yake ikaita tena, alikuwa ni Derrick aliyempigia. Akapokea.

******************

"Nitakupigia baadae Retha. Love you" Edrian akakata simu bila kusubiri jibu la Aretha na akageuza vyema kiti chake kumwangalia mgeni aliyesimama mbele ya meza yake.

"Samahani Mr Simunge, sikukusudia kukatisha maongezi yako" akasema Renatha asijue akae au aendelee kusimama

"Hujayakatisha Renatha, ni mimi nimekata simu ilinikusikilize." Edrian akamwangalia akiwa tayari kumsikiliza

Renatha ambaye kwanza alishtushwa na kumsikia Edrian akiita jina la Retha na zaidi sana kusikia akimwambia "love you". Alitamani kumjua huyo mtu ni nani maana mpaka sasa alimfahamu Joselyn na vituko vyake.

"Renatha" Edrian akamtoa kwenye mawazo yake

"Aaahm" Renatha akashtuka

"Samahani, Mr Simunge nimepata taarifa mna mkutano wa bodi" Renatha akazungumza huku akisogea kilipo kiti akae..

"Mmmmm" Edrian akaguna na macho yake yakamwangalia kwa ukali Renatha kiasi cha kumfanya mwili wake kusisimka

"Àaaaaah inaonekana haukupenda niju__"

"Renatha" Edrian akamkatisha

Renatha alipomwangalia Edrian baada ya kuita jina lake, kidogo ageuke na kukimbia

"Yes boss" akaitika kwa kukaza sauti

"Unataka nikusaidie nini?" Edrian akauliza kwa sura ya kikazi ambayo ilimfanya Renatha ashikwe na kigugumizi

"Mr Simunge, ninaweza kupata kibali cha kupitia tathmini ya upatikanaji wa maeneo mapya ya uchimbaji?" Renatha akajikaza na kumwambia Edrian

"Kwa nini?" Akauliza Edrian huku akimkazia macho Renatha ambaye naye hakujaribu hata kupepesa macho ili asionekane kutishwa na hali iliyokuwa mbele yake

"Nafikiri kuna kitu naweza kufaidia SGC" akajibu Renatha

"Kwa nini unataka kutusaidia Renatha?" Akauliza Edrian huku akiweka mikono yake miwili juu ya meza.

"Na kwa nini nisiwasaidie kama ninaona naweza kufanya hivyo?" Renatha akarudisha swali kwa Edrian, akaketi huku akimtazama

Edrian akanyamaza kwa sekunde chache akiendelea kumwangalia Renatha. Akashusha pumzi na kuegama kwenye kiti

"Renatha, why are you here" akamuuliza tena uso wake ukiwa na muonekano ule ule..

"Mr Simunge, nimeomba kuona tathmini ya maeneo mapya mnayoyaandaa kwa ajili ya operasheni. It's a request and not an order sir" Renatha akamjibu

"Hapana, hilo eneo si sehemu ya kazi yako Renatha" Edrian akamwambia

"Basi sawa bosi. Ila ukiona umuhimu wa msaada wangu usisite kunijulisha" Renatha akainuka huku akitabasamu

Edrian akamwangalia sana Renatha akishangaa ni nini hasa kilimsukuma kufikiri juu ya maeneo mapya.

Renatha akapiga hatua kutoka, lakini alipofika mlangoni akageuka na kumwangalia Edrian,

"I am not your enemy boss" akatabasamu na kutoka mle ndani akimuacha Edrian katika kutafakari nini kinaendelea ndani ya binti yule.

"Kwa ujasiri tu nakukubali lakini siwezi kukuamini katika hili" akawaza taratibu Edrian.

Akaendelea na kazi huku akitupia jicho kwenye saa yake, akatabasamu alipokumbuka maneno ya Aretha alipomuuliza kama amekula.

"Japokuwa muda umeenda lakini ngoja nile walau hata matunda" akawaza na kisha akainua simu kumuagiza Loy