webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

NIFIKIRIE KWANZA

Aretha alitulia akitazama mandhari safi iliyovutia kutoka kwenye baraza la juu la jengo hili la Ashanti. Akiwa mawazoni juu ya picha aliyokusudia kuipiga simu yake ikaita alipotazama haikuwa namba anayoifahamu, akasita kupokea huku akiiacha iite kwa muda hadi ikakata. Lakini simu iliita tena ķwa ile namba, na mara hii akaamua kupokea,

"Hellow" akaita

"Aretha, unaendeleaje?" Sauti ya mwanaume upande wa pili ilisikika

"Aaah naendelea vizuri, naongea na__" kabla ya kumalizia akakatishwa

"BM hapa, nimeona nikujulie hali" sauti ya BM ilikuwa ya utulivu kiasi cha kumfanya Aretha kupunguza wasi wasi

'Aah Asante niko salama" akajibu Aretha asijue nini aseme, kimya cha sekunde chache kikapita na alipotaka kuongea Aretha, wakajikuta wakianza kwa pamoja

"Endelea tu" BM akamsihi Aretha

"Ahhh, mm.. Asante kununua zile picha" Aretha akamwambia

"Oooh ninathamini juhudi zako naamini utafika mbali. Kulikuwa hakuna sababu ya kuanza kukukatisha tamaa." BM akamwambia..

"Nashukuru" Aretha akashukuru,

"Kuna kazi nafikiri unaweza kunisaidia kuifanya Jumamosi kama utaona vyema" BM akaleta wazo lake

"Mmmh kazi! Aa__"

BM akamuwahi Aretha "Kabla haujaikataa naomba unisikilize kwanza" akamsihi

Aretha akanyamaza kumpa nafasi aendelee

"Ninahitaji picha tatu muhimu sana ambazo nitazisafirisha nje ya nchi kwa ajili ya mnada ambao kampuni yangu inausimamia. Na kwa namna niliziona picha zako nina uhakika tunahitaji talanta kama yako. Tutakulipa pesa yoyote utakayotaka" BM akapumua kidogo huku akisubiri mrejesho wa Aretha

"Lakini mimi sina ujuzi mkubwa kama Melissa na Beruya, kwa nini usiwasiliane na hao?"akauliza kwa mshangao

"Aretha kila mchoraji ana namna ya kuchora na kuwasilisha ujumbe wake, namna yako kwa sasa tunataka kuiingiza kwenye soko. Au wewe hauhitaji?"

" Ahhh hapana. Samahani lakini naomba nifikirie kwanza nitakujulisha" Aretha akajitetea

"Sawa, naomba nikupe masaa mawili utanijulisha"

"Haya. Asante" Aretha akashukuru na wakati huo BM alikata simu.

Mara alipokata simu akatafakari kuhusu nafasi hiyo ambayo aliona ni fursa njema kwake. Pamoja na akili yake kukubaliana na fursa hii bado ndani ya dhamiri yake alihisi kutahadharishwa. Alipowaza kumshirikisha Edrian hofu ikamjaa akikumbuka namna ambavyo walitofautiana wakati wa onesho.

"Hawezi kukubali" akawaza

Meseji ikaingia kwenye simu yake,

"Princess, Loy anakuja huko, naomba uingize taarifa zako kwenye hiyo kompyuta. Ni muhimu. Usisahau kula matunda" Nakupenda."

Akatabasamu kisha mkono wake ukachukua ndizi akamenya na kuanza kula huku akimsubiri Loy.

**************

Edrian alihakikisha anafanya kazi zake kwa haraka baada ya kutuma fomu za maombi ya hati ya kusafiria kwa ajili ya Aretha. Alipohakikisha hana kazi nyingine tena, akasimama na kujinyoosha kisha akaweka vitu vyake sawa juu ya meza. Akaelekea maliwatoni.

Alipotoka akachukua mfuko ambao aliuagiza masaa matatu nyuma pamoja na simu yake akatoka. Loy naye alikuwa akiweka vitu vyake sawa ili kuondoka,

"Allan amesharudi?" Akauliza huku akitaka kuelekea ofisini kwake lakini Loy akamjulisha kuwa ametoka nje kiofisi.

"Okay. Jioni njema Loy" akamuaga.

"Nashukuru bosi"

Edrian akaelekea ilipo lifti na kuingia, akaelekea juu alipo Aretha. Mara mlango ulipofunguka Edrian akauangalia tena ule mfuko na kutabasamu halafu akapiga hatua nje ya lifti. Akapanda ngazi na alipokaribia kumaliza ngazi akasikia sauti ya Aretha akiongea na simu. Ghafla akahisi wivu akaamua kusimama pale ili asikie aliongea na nani..

"Sawa nitajitahidi muda huo niwepo" sauti ya Aretha ikasikika

"Haya, Asante kwa kunishirikisha fursa hii" aliendelea Aretha kisha wakaagana na baadae akashusha pumzi kwa nguvu.

Edrian akaelekea alipo Aretha, "huu utulivu nikajua umelala kabisa" akamwambia huku akitabasamu

Aretha akashtuka baada ya kumuona, akatamani amuulize kama alisikia maongezi yote aliyokuwa aliongea

"Aaah umenishtua" akamwambia huku akiinuka

"Hahaha kwani ulikuwa unaniwaza?" Akacheka

"Hapana aa namaanisha ndio lakini umetokezea tofauti na matarajio yangu.. umemaliza kazi?"Aretha akamuuliza mara alipomkaribia