webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

NI SHWARI

Li hakuweza kulala usiku kucha toka muda ule aliomfikisha Beruya nyumbani kwa mama yake. Chumba alicholala kilikuwa ni chumba kilichotumiwa na Li wakati wote walipoishi kwenye nyumba hii. Alimtazama Beruya ambaye alilala pasipo kuwa na ufahamu wowote juu ya mambo yaliendelea barabarani.

"Mhhhhh" akashusha pumzi mara aliporejea na beseni lenye maji na kitambaa safi laini akamfuta jasho ambalo lilianza kuonekana usoni kwa Beruya..

Huku akiwa na wasi wasi akachukua simu na kumpigia Dokta Brianna akamueleza hali ilivyo, kwa sasa lakini Dokta akamuondoa shaka

"Li hiyo dawa niliyoichoma ndani ya dripu inapambana na ile ambayo alichomwa mwanzo hilo joto litakaa vyema. Fanya kama nilivyokuagiza, tumia maji na kitambaa kumfuta taratibu mwili wake utarejea"

Li akamshukuru kisha akakata simu, "hili zoezi sikujua kama lingekuwa gumu, namuombea apone haraka la sivyo itakuwa shida" akawaza kwa sauti.

Mara alipofika nyumbani na kumtaarifu mama yake juu ya ujio wa Beruya na hali aliyokuwa nayo, mama yake alimshauri amtafute daktari waweze kuangalia hali yake. Walifanya hivi baada ya kujaribu kumuamsha Beruya lakini hawakufanikiwa, hawakujua msaada wa kumpa.

Dokta Brianna alipofika alifanya uchunguzi wa haraka na akagundua kuwa Beruya alichomwa dawa ambayo inafanya awe katika hali ya kupoteza fahamu kwa masaa mengi. Ili kumrudisha alihitaji kumwekea dawa nyingine ambayo itapunguza taratibu utendaji kazi wa ile ya kwanza. Akamwekea dripu la maji na kisha akachoma dawa mpya ndani yake. Dripu ile ilitona taratibu kuingia mwilini kwa Beruya..

Li aliendelea kumfuta taratibu, alitamani angekuwepo Coletha angempa ile kazi lakini hakuwa nyumbani ambako aliishi nao. Hapa palikuwa kwa mama yake na muda ambao alitumia kumsaidia mara alipofika hakutaka kumsumbua tena, japokuwa mama alimwambia amuashe ikiwa angehitaji msaada zaidi.

Wakati akimfuta taratibu kwa kile kitambaa laini aliona akikunja nyusi kama mtu aliyekuwa kwenye ndoto ya kutisha na kila mara alipofanya hivyo alitoka kijasho kwenye paji lake la uso!

"Nini kinaendelea Beruya" akamuuliza huku akiwa na hakika hatoweza kupewa majibu yoyote. Akamwangalia namna alivyolala akasikia funda zito limemkaba kooni. Huruma ikamshika huku akitafakari mambo mazito ambayo ameyapitia mara alipochomwa sindano ile. Hasira zikamshika alipomfikiria Damian

"Unakuwaje daktari na ukatili wa namna you?"

Ghafla mikono ya Beruya ikarushwa hewani kama mtu aliyekuwa akijitetea asiumizwe, beseni ambalo Li alilishika likaanguka pembeni. Li akamuwahi na kumshika mkono ule ambao sindano ya dripu iliwekwa. Akamshika vyema huku akiinuka na kuketi kitandani akamshika mikono yote miwili.

Machozi yakatiririka pembeni ya macho ya Beruya, Li akatamani angesikia nini kinachomfanya atoe machozi yale walau amfariji lakini asingeweza kwani Beruya alikuwa katika usingizi ambao bado ulikuwa na jinamizi likimuwinda!

Akanyoosha mkono kuchukua kitambaa laini kwenye boksi lililokuwa pembeni ya kitanda. Akamfuta machozi yale "Ni shwari Beruya usiendelee kulia." Kama vile Beruya alisikia maneno ya Li, machozi yakaacha kutiririka.

"Thank you" Li akajikuta akisema maneno yale, sauti ya mtetemo wa simu yake ikiita ikamshtua akaivuta kutoka kwenye meza iliyokuwa pembeni

Alipoangalia kioo cha simu yake, Edrian kaka yake akipiga simu ile, akapokea ambayo ilipigwa kwa mfumo wa video

"Brother" akaitika Li

"Uko na Beruya?" Ed akauliza mara alipomuona kwenye kile chumba ambacho alikifahamu

"Ndio bro, yuko hapa japokuwa hali yake sio njema ila Dokta Brianna amesema ndani ya siku mbili itarejea vyema" Li akajibu huku akiiweka vyema kamera

Kimya cha sekunde kilipita kisha Ed akaendelea "ilikuwaje, nambie?"

Li akamsimulia kwa ufupi jinsi ilivyokuwa na namna ambavyo akimuacha Captain kumalizia yaliyosalia huku yeye akiwahi kumsaidia Beruya..

"Asante sana brother!" Akashukuru Ed kisha akaongeza, "Mwache akae hapo mpaka nitakaporejea na kama atasisitiza kuondoka usimzuie, isijekuwa tunalazimisha mtu pasipo kujali maamuzi yake"

"Sawa brother. Mmefika Kuala Lumpur?" Akauliza Li huku akitazama kwenye kioo cha simu yake