webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

MWENYE BAHATI

"Retha unaweza kuongeza, don't be shy" Ed akamwambia Aretha baada ya kuona namna alivyokifurahia chakula.

"Aahh hapana nimetosheka Rian..umeniwekea hadi cha kweli aa yatosha" Aretha akamkatalia kwa aibu, ni kweli chakula kilikuwa na ladha nzuri, mara zote Ed alichukua sehemu chakula na kuweka kwenye sahani yake.

"Tuchukue na cha baadae basi princess" kwa kujua Aretha alifurahia chakula kile, Edrian alitamani kumfurahisha.

"Hapana Rian nimekula leo, siku nyingine nitakula pia" Aretha hakuona sababu ya kuchukua kingine maana aliamini ipo siku watakuja tena pale

"Sawa, nitajitahidi kukuleta hapa" Ed akatabasamu, akaingia kwenye simu yake na kufungua ukurasa wa mgahawa ule, akafanya malipo. Wakawa wakisubiri risiti ndipo waondoke..

Wakaingia wanaume wawili ambao walionekana kuwa na hadhi ya juu kwa ule unadhifu waliokuwa nao kwa mavazi na hate muondoko wao. Mmoja alivaa suti safi yenye rangi ya kijivu huku mkononi saa yake ilionesha kuwa ya gharama kubwa. Mwenzie alivaa shati nyeupe ya mikono mifupi na suruali ya kadeti nyeusi. Kwenye shingo yake kulikuwa na mkufu ulioonesha kuwa na thamani ya dhahabu. Wakapiga hatua kuelekea kwenye meza ambayo ilikuwa karibu na ile waliyokaa Edrian na Aretha.

Lakini walipomuona Ed wakasogea kumsalimia ikionesha kuwa walifahamiana. Uso wa Ed ulibadilika kutoka kwenye tabasamu pana lililojaa usoni wakati akiongea na Aretha hadi kwenye uso wa kikazi zaidi..

"Simunge good to see you" akasema yule aliyevaa suti! Akanyoosha mkono ili kumpa Ed ambaye hakuupokea akabaki na uso usio na changamko lolote akimwangalia.."Good to see you Salim"

"Nakuona una mwanafunzi hapa.. unajaribu kuanza darasa au waanzisha chuo" Salim akamwambia Ed akiwa na tabasamu la dhihaka akitoa macho yake kumuelekea Aretha ambaye hakuinua macho kuwaangalia wageni wale

"Hello mwanafunzi" Salim akasalimia kwa dhihaka kisha akamgeukia mwenzake ambaye alikuwa na tabasamu kama lake "Idris, rafiki yetu anapata mawazo kutoka kwa mwanafunzi ya kuwekeza"

"Sure, Mwenye enzi Simunge anapata mawazo kutoka kwa mwanafunzi wa kike mgahawani" Idris akajibu kwa dhihaka

Edrian akawaangalia lakini kabla ya kusema kitu mhudumu akamletea risiti. Akainuka na kumshika mkono Aretha, "twende Retha"

"Hahaha mighty Simunge umemtupilia mbali mwanamke wa hadhi yako ili kuvumbua nini kwa mwanafunzi!" Salim akacheka na kuongea japokuwa sauti yake haikusikika sana

"I wonder bro, unatupa dhahabu unakumbatia mchanga" Idris naye akaongeza maneno huku akicheka

Edrian ambaye alikuwa amepiga hatua chache akageuka kutaka kuwaambia kitu lakini mkono wa Aretha ulimzuia, alipogeuka kumwangalia usoni, macho ha upole na tabasamu laini vikabadilisha hasira iliyoanza kufuka kama moshi kifuani kwake.

Akawaangalia Salim na Idris akatabasamu na kumshika kiunoni Aretha wakaondoka. Baadhi wa watu wachache waliokuwa wakila waligeuka kuangalia. Hawakusikia kilichoongelewa lakini kuondoka kwa Ed kwa namna ile kulivuta hisia zao.

Walipofika garini, Edrian akamwangalia Aretha na kumwambia "Asante princess..samahani kwa maneno ya wapuuzi wale"

Akatabasamu na kumjibu, "usikasirike Rian, watu husema kile wanachotaka kusema, huwezi kuwazuia. Mama husema kuwa " usizuie watu kukurushia mawe, ila unaweza kuamua nini unafanya na mawe unayotupiwa"

"Ahmmm" Ed akamwangalia na furaha yake ilikuwa kuu, "Retha..unanipa kujisikia kwenye bahati sana kuwa nawe"

Aretha akamwangalia Ed usoni kisha akamwambia "mimi ndiye mwenye bahati kwa kuwa nimekubalika nawe na___"

Ed akamvuta na kumkumbatia kwa nguvu Aretha ambaye alishtushwa na kumbatio lile. Akabaki kifuani kwa Ed huku akisikiliza mapigo yake ya moyo yalivyodunda..

"Retha, natamani ningekuona siku ile, kuna mambo yangekuwa tofauti na yalivyo sasa. Wewe umebeba maisha yangu sasa.. please love me this and that much"

"Rian...tuko kwenye gari watu wanaweza kutuona" Aretha akamtahadharisha Rian

"Unajua kitu nachotamani kufanya sasa Retha?" Ed akamuuliza kwa sauti ya utulivu

"Mmmmmh"

"Nataka watu wote waone kuwa nimependwa na mimi ninaweza kupenda" mikono ya Ed haikumuachia bali aliendelea kumbusu kichwani