webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

MNAFAHAMIANA?

"Aretha uko salama?" Akauliza Coletha huku akimpa maji pale alipoketi. Aretha akayapokea na kunywa kimya na alipomaliza akarudisha chupa kwa Coletha.

Macho yake akayainua kuangalia kule picha zilipokuwa, machozi taratibu yakaanza kumtoka.

Wakati huo huo Derrick alikuwa akizungumza na Yassin meneja wa Beruya ambaye naye alikuwa amechanganyikiwa kwa kile ambacho kilifanyika kwenye picha zote pale ukumbini. Watu wengine walianza kutoka, malalamiko yaliendelea kusikika hapa na pale wengine wakimfuata Yassin kutaka kujua hatma ya onesho hilo.

Edrian akarudi kwa haraka kwa Aretha ambaye hakuongea chochote zaidi ya kumwangalia tu usoni na kulia.

"Retha please don't be hard on yourself, it's goin to be okay" akajaribu kumbembeleza, lakini sauti ya kipaza sauti ikawashtua

"Mabibi na mabwana naomba usikivu wenu"

Edrian hakujaribu kuinua macho kumwangalia aliyeongea, alimuweka Aretha kifuani kwake huku machozi yakilowanisha shati yake na kumfanya kusikia ubaridi ukifikia ngozi yake. Sura yake ilibeba mfano wa bomu lililokuwa tayari kulipuka

Ukumbi ulipopata utulivu akaendelea kuongea, "kuna wakati vitu huwa vinatokea nje ya matakwa yetu, lakini haimaanishi kuwa hakuna wema tunaoweza kuuvuna." Akaangalia mahali alipokuwa Aretha na Ed lakini wao hawakumuona sababu walimtega mgongo...

Akaendelea, "Hizi picha zinazoonekana kuchanwa katikati zinabeba hadithi ambayo mimi nataka niinunue kwa gharama yoyote" Derrick na Yassin wakashtuka baada ya kusikia maneno yale. Derrick akamkumbuka mtu yule lakini kwa kuwa bado akili yake iliwaza kilichotokea hakujali sana maana aliona amewasaidia kuokoa jahazi lililoelekea kuzama! Yassin akaachia tabasamu la matumaini.

Edrian aliposikia maneno yale akageuka amuone aliyeongea, ghafla sura yake ikabadilika lakini akajikaza akiendelea kumkumbatia Aretha ambaye aliificha sura yake kifuani kwake.

Watu waliokuwa ukumbini wakageuka na kuangalia zile picha huku minong'ono ikiibuka hapa na pale maana ilikuwa ni vigumu kuona uzuri. Ni wazi kabisa aliyechana alitumia kisu kikali na kwa kila picha alichana alama ya X katikati ya picha.

"Nitanunua picha tano za Aretha ambaye ni mchoraji chipukizi ili kutomkatisha tamaa na tatu za Beruya ambaye najua atainuka tena. Kuna yeyote anayeweza kuniunga mkono? Karibu" Akamaliza huku mwanaume huyu ambaye muonekano wake uliwafanya watu waliokuwa ukumbini kumsikiliza.

Yassin aliposikia maneno yale akaelekea aliposimama mwanaume huyu ambaye macho yake yalielekea kule alipokuwa Aretha, " Nashukuru sana BM kwa kuunga mkono juhudi za Beruya. Picha hizi zote mpaka muda alipoondoka Beruya zilikuwa salama. Hatujui kilichotokea. Lakini nina uhakika hatutaruhusu tukio hili liwe sababu ya kutuzuia kuendelea. Tutafuatilia kujua nani alihusika. Kwa atakayetaka hizi picha anaweza kuonana nami au mwenye beji ya mauzo" Yassin akamaliza

Aretha aliposikia jina la BM likitajwa akashtuka na akajitoa kifuani kwa Edrian kisha akainuka na kutazama jukwaani. Wakati huo BM alianza kushuka ngazi kuelekea alipokuwa Aretha.

Derrick alipoona muelekeo wa BM akasogea kwa haraka alipokuwa Aretha na wakati huo Edrian alisimama pembeni yake.

Edrian alipoona Aretha akijaribu kutabasamu huku akimuangalia BM, akahisi ngumi nzito ya wivu ikigonga moyoni mwake. Akainama kwenye sikio la Aretha akamuuliza taratibu japokuwa Derrick aliyekuwa amesimama karibu naye alisikia

"Mnafahamiana Retha?"

"Aaaaahm" akashangaa na kutaka kumjibu Ed lakini alichelewa maana tayari BM alikuwa mbele yao..

"Mr Simunge sikuwahi kujua unavutia na sanaa hii ya picha!" BM akamtania Ed huku akinyoosha mkono kumsalimia

"Mmmmmm" Edrian akaguna lakini akanyoosha mkono wake kumsalimia

"Aretha pole kwa kilichotokea, lakini nataka nitunze kumbukumbu ya huu mwanzo wa safari yako" BM akamwambia Aretha huku akitaka kumgusa begani, lakini Edrian akamvuta ubavuni kwake

Derrick akaingilia kati baada ya kuona hali ya kaka yake ikibadilika

"Asante kwa kujitolea kununua picha za Aretha, hayuko vizuri kwa sasa, naweza kuongea nawe, mimi ni meneja wake"

"Ooooh ni sawa" BM akamjibu Derrick kisha akamgeukia Aretha