webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

MKONO WAKO UMEFANYA HAYA

"Retha, samahani nilipata simu ya dharura ofisini na sasa niko njiani naelekea huko" Edrian akaongea na simu mara tu alipoingia kwenye gari...

"Kuna tatizo kubwa?" Akauliza Aretha kwa wasiwasi

"Sijui, lakini mfumo wa mawasiliano umezima ghafla wakati ambao kuna ndogo uko safarini. Naomba unipe muda nitakutafuta nitakapomaliza."

"Sawa." Aretha akajibu na kukata simu.

Akaamuru simu impigie Captain, "Vipi umefikiwa wapi?"

"Sio jambo la kawaida mfumo kuzima pasipo kutoa onyo. Nafanyia kazi kaka"

"Niko njiani nakuja, tafuta namna nyingine ya kuwapata walioko njiani na mzigo" Ed akajibu huku uso wake ukijikunja. Kwanza alichoshwa na kuvurugiwa ratiba yake ya mapumziko. Ratiba yake na Aretha siku za mwisho pale Singapore iliwapa nafasi kidogo ya kupumzika. Alihitaji muda huu ili kujiweka sawa kabla ya kurejea katika majukumu yake ya kuja siku.

'Nini kinaendelea hapa?' Akawaza.

**********

"Habari ya mchana Loy" Ed akamsalimia Loyce ambaye aliinama kwenye kompyuta akifuata maelekezo ya Captain ambaye alikuwa ofisini kwa Alphonce

"S-salama bosi, nikulet____" Loy akataka kusimama lakini kabla ya kufanya hivyo Ed alikuwa ameingia ofisini kwake

"Mhhh leo siku itakuwa ndefu" Loy akasema huku akiketi kwenye kiti

Ed akaelekea kwenye kabati lake lililokuwa karibu na mlango wa kuingia kwenye maliwato. Akafungua mlango wa upande wa kushoto kisha akabonyeza kitufe kwa juu ya mbao. Kukafunguka sehemu ndogo kama kisanduku cha hazina, akaweka kidole chake na kisha akaingiza namba, kikafunguka. Akatoa kifaa kidogo kama kitunza taarifa akakiingiza mfukoni. Akafunga na kisha akatoka ofisini kuelekea ofisini kwa Alphonce huku njiani akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa SGC ambao walifurahi kumuona..

"Habari zenu!" Akasalimia mara alipoingia

"Salama kaka" wakajibu huku Alphonce na Allan wakiinua nyuso zao kumtazama, lakini Captain hakutoa macho yake kwenye kompyuta.

"Tumepata nini hadi sasa?" Akauliza Ed huku akitamani aambiwe limeishamalizika..

"Inaonesha tumetembelewa na kirusi mpya ambaye nina uhakika amepandwa na mtu makusudi ya kuharibu mfumo wa mawasiliano" Captain alijibu huku akiendelea kubonyeza vitufe kwenye kompyuta.

"Unaweza kuangalia alipandwa kutokea wapi?" Akauliza Alphonce

"Nafikiri itakuwa vizuri" akajibu Ed

Captain akainua kichwa na kumtazama Allan kisha akaendelea na kuchapa namba kwenye kompyuta ambazo kwa mtu mwingine angedhani hajui alichofanya.

Baada ya dakika kumi, Captain akaachia tabasamu na kubonyeza kitufe cha kuingia mara kompyuta ikazima na kisha sekunde thelathini ikawaka tena..

"Tumerudi" akamwambia Edrian ambaye aliketi kwenye kiti karibu na mlango..

"Allan fuatilia na watu wa G-Town"

Allan aliposikia maelekezo ya Ed akawa kama mtu aliyezinduka usingizini, akainuka kiunyonge na kuelekea ofisini kwake

Akabaki Alphonce, Captain, Silvia na Edrian.

"Umefanikiwa kupata chanzo cha huyo kirusi?" Akauliza

"Nafanyia kazi bro, ila nipe dakika chache nitamaliza kazi" Captain akamjibu

Allan alipoingia ofisini kwake akachukua simu yake na kumpigia Renatha,

"Salama Renatha, naomba uniambie ukweli kama hauhusiki na kupanda hicho kirusi?"

"Kirusi gani?" Akauliza Renatha kwa mshangao.

"Usiniigizie tafadhali nakuomba, hujui kirusi kilichofunga mawasiliano na ofisi za G-Town" sasa sauti ya Allan ilibeba hisia za hasira

"Allan, nimeomba ruhusa nipumzike, sio kuanza kushtakiwa kwa makosa nisiyofahamu" Renatha naye akajibu kwa hasira

"Naomba isiwe ni mkono wako umefanya haya Renatha." Allan alipomaliza akakata simu na kushusha pumzi kwa nguvu. Akaegemea kwenye kiti lakini akakumbuka maagizo ya Ed.

Akaingia kwenye mfumo wa mawasiliano na kisha akawatafuta watu wa mgodi wa SGC G-Town.

Baada ya dakika tano Allan alipata taarifa mbaya zaidi juu ya ndege iliyobeba mzigo kupoteza mawasiliano na kutojulikana ilipo.

Allan sasa alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa akijaribu kuwasiliana na watu ambao aliamini wanaweza kusaidia kufuatilia taarifa za awali za ndege.

Akampigia akampigia Ed ambaye bado alikuwa ofisini kwa Alphonce. Wakakutana ofisini kwa Ed,

"Tunatakiwa kuondoka sasa hivi"