webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

HISIA TOFAUTI

Ed aliinuka tayari kumtoa mgeni, lakini akakumbuka ule mfuko uliokuja na biskuti

"Aretha subiri" Ed akamshika mkono Aretha aliyekuwa amepiga hatua mbele yake na kumfanya ageuke nyuma.. Kitendo kile ni kama kiliamsha hisia za Ed na kukumbuka siku tatu nyuma.

Wakati huu Aretha alibaki amesimama akiuangalia mkono wa Ed uliomshika na hakujua namna gani angepata kuelewa kile alichohisi mwilini mwake.

Ed hakujua ni sekunde ngapi zilipita akiwa ameushika ule mkono wa Aretha mpaka aliposikia sauti yake ikimsemesha

"Umeniita Edrian"

"Oooh yes.. " alishtuka na kuuachia mkono wa Aretha. Akarudi nyuma na kuchukua mfuko mweupe wenye boksi la biskuti na kumkabidhi

"Kamalizie na hii hapa"

Aretha alipokea na kushukuru huku akiangalia ndani ya mfuko na kufanya tabasamu kuonekana usoni kwake lakini likayeyuka ghafla, akamwangalia Ed

"Mbona umenipa zote? Na wewe je?" Aliuliza Aretha

Ed akamwangalia Aretha kwa hisia za ajabu kisha akaendelea

"Worry not, huwa sipendi vitu vya sukari nyingi" alijibu

"Oooh.... sawa. Asante sana" lilikuwa jibu la Aretha

Ed akatangulia ili kumfungulia mlango mgeni wake, lakini mkono uliposhika kitasa akakumbuka, akaingiza mkono mfukoni kutoa pochi yake ambapo alitoa business card yake na kumpa Aretha kisha akasema

"Utanijulisha ukiwa tayari nione picha unazochora"

Akapokea ile kadi, na kushukuru kisha akaiweka kwenye begi lake.

"Unaelekea wapi kwa sasa, naweza kukusogeza maana nina ratiba ya kutoka" aliuliza Ed ambaye wakati huu alijaribu kutafuta namna ya kumuomba namba yake ya simu lakini alihisi ataonekana vibaya mbele ya binti huyu.

Aretha aliwahi kujibu

"No...no no usijali nitaenda tu mwenyewe, naenda nyumbani, hata hivyo kutoka hapa sio mbali na kituo cha basi"

"Basi sawa." akajibu Ed kinyonge, akafungua mlango na Aretha akatoka.

Wakati huo Ed aliangalia kwenye mlango wa Allan ili asije kutana na mdogo wake... Akachukua hatua kumtoa Aretha ambaye alielekea kwa Loy kumshukuru.

Ed akabaki akimsindikiza kwa macho wakati akifungua mlango na kutoka huku akimpungia mkono.

Macho ya Loy yalikuwa kwa bosi wake, akishangaa tabasamu lake ambalo lilikuwa wazo usoni pake. Kwa kawaida Ed huwa na tabasamu hilo pale ambapo mradi wake unapofikia upeo wa mafanikio, mbali na hapo ni mara chache kumuona akitabasamu hivi.

Ed aligeuka na kumwangalia Loy ambaye alikwepesha macho na kuyarudisha kwenye kompyuta iliyokuwa mbele yake kuendelea kuchapa barua za ofisi.

****************************

Ofisini kwa Allan...

"Comrade umemuona mwokozi wako?" Aliuliza Allan akamwangalia Linus ambaye alikuwa amekaa kizembe kwenye kochi la mtu mmoja pembeni ya meza

"Ha ha ha nimemuona" alijibu Li kisha akaendelea huku akikaa vyema sasa

"Kinachonipa raha ni muonekano wa bro baada ya kumuona... sijui nini ambacho anakiona kwa huyu binti lakini naweza sema kinamuathiri"

"Heh?" Alishangaa Allan,

Linus akatulia kisha akaendelea,"Na hivyo kinachomuathiri bro, ndio strong point ya Aretha"

"Comrade unawaza nini tena?" Allan aliuliza baada ya kuona hampati vyema Li

"Sikia Allan nachosema ni hiki; Joselyn ni mzuri wa sura kuliko hata Aretha, lakini kwa macho yangu sijawahi muona bro anakosa maneno kwa uwepo wake"

"Mhhhh?" Aliguna Allan kumuashiria aendelee,

"Huyu Aretha ni sawa na sumaku na bro ni chuma, ngoja tuone. Amechukua muda mrefu sijui wanaongea nini?"

"Ha ha ha comrade unasahau patience is the key" alijibu Allan akicheka taratibu

"Haaaa, sawa Comrade, nimempenda yuko so simple ila nahofia Joselyn na baba yake, hawataruhusu amsogelee Ed wakijua nini kinaendelea." Alisema Li huku akitafakari sana

"Usijitaabishe sana Comrade, acha tumwamini bro, kama atakuwa na hisia tofauti kwa Aretha hatokubali kuziacha japokuwa he is a man of his word." Alimtia moyo Li

"Exactly, hilo ndilo linanikatisha tamaa, a man of his word, na ameshaahidi kumvisha pete Lyn, atakubali kuyapinga maamuzi yake mwenyewe?" Aliuliza Li huku akiegama tena kwenye kochi..

Allan akanyamaza akimwangalia rafiki yake ambaye alijua kwa hakika anaumia kwa yale ambayo Joselyn anayafanya. Hakujua kwa nini ila alihofia familia yake kuhusiana na Martinez