webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

DO I LOVE HER

"Champ, ni wewe pekee unaweza kuchambua kile unachokihisi, lakini kuna mstari mwembamba unaotenganisha kile kinachoendelea ndani yako. Unahitaji kuiambia nafsi yako ukweli. Je ulimpenda Lyn kwa dhati ya moyo au la?"

Maneno haya kutoka kwa Brian yalimsababisha Ed kuinama chini taratibu akishusha pumzi. Kimya cha dakika kadhaa kilipita na Bri alimalizia chakula chake huku akimpa rafiki yake nafasi ya kufikiri.

"Champ, ninaweza kusema ukweli huu, kwa Lyn it was easy! I didn't chase her, but kwa Aretha ninataka kumfuata, nataka kujua kila kitu kinachomhusu yeye. Ni mimi ndio namtaka zaidi. Ni mara mbili tu nimeongea nae lakini nataka kuongea nae tena na tena. Nikiongea na Lyn nahisi kama ninamdanganya maana moyo hautaki kusema maneno ambayo natamani kusema kwa Aretha! Napata shida kutulia kila nikimuwaza. Nipe maana moja ya haya nayofanya Bri, do I love her?"

Ed alinyanyua glasi ya maji na kunywa kisha akaegama kwenye kiti huku akimuangalia Brian ambaye alikuwa makini kumsikiliza.

Alimshangaa sana rafikiye, sababu hakuwahi kumuona hivyo akiwa na Joselyn. Alichofanya ni kumtambulisha kwake walipokutana kwenye sherehe za uzinduzi wa programu ya mabadilishano ya utaalam kati ya City Hospital na Country C. Brian alimfahamu kwa ufupi hapo lakini hakuwahi kumuona Ed akimsimulia mambo haya katika uzito anaofanya sasa kwa huyu Aretha.

"Kama rafiki yako, natamani kukuona unafanya maamuzi sahihi linapokuja suala la mwenzi. Kabla sijakupa maana ya kile kinachoendelea, mfahamu Aretha. Tafuta muda kumfahamu, take her as a friend you have met!. Kisha tuone maendeleo"

Ed alisikia ushauri wa rafiki yake Brian, kisha akauliza

"Kwa muda gani Champ? Nina wiki sasa mbele kumtambulisha Lyn. Na kama unavyomjua Lyn atatafuta kujua why namfuata huyu dada?"

Brian alishusha glasi na kutabasamu,

"Muda utaamua wewe, na ukiwa karibu nae utajua namna ya kukabiliana na Lyn, maana sitaweza kukwambia nini ufanye kuhusu kumtambulisha Lyn, unamjua na unaweza kukabiliana na chochote ikiwemo kusogeza mbele utambulisho... na kama utagundua hisia zako ni halisi kwa Aretha kuliko Lyn, you are a gentleman deal with it respectively. Talk to her. Mwambie ukweli bila kupepesa lakini kwa heshima na upole".

Mazungumzo haya yalimuacha Ed akiwa na ahueni ya kutosha kuliko alivyokuwa siku chache nyuma. Alishukuru sana kuwa na Brian, ambaye amekuwa msaada kwake mara zote kunapokuwa na changamoto za kimaisha. Hakufahamu kuwa Brian alikuwa anafahamu taarifa ya Aretha mapema kabla ya kumtaarifu. Linus alishampa hali ilivyo tangu siku ya kwanza alipomuona Aretha.

Walipomaliza alielekea nyumbani huku akikusudia moyoni wikiendi kumfuatilia Aretha. Akiwa njiani aliwaza kuitumia wikiendi hii pia kutengeneza mahusiano yake vyema na mdogo wake Derrick. Akachukua simu yake na kupiga namba ya Derrick, baada ya kuita kwa muda ikapokelewa. Mazungumzo yao yalikuwa mafupi lakini yalimpa Ed kujisikia vyema maana Derrick alikubali kuja nyumbani jumamosi kuonana nae.

Moyoni alihisi ushindi na furaha kabla kioo cha simu yake kuwaka kuonesha kuna mtu alitaka kuongea nae. Alipoangalia alipokea haraka huku mkono ukibaki kwenye usukani.

"Sema Captain" alisema Ed mara baada ya kupokea huku akiweka sauti kusikika

"Mkuu, kuna taarifa za kuvutia kutoka kwa Martinez" upande wa pili ulisikia

"Nambie" Ed alimpa ruhusa kuendelea!

"Our suspicions were true, Martinez ana kupe pale Boric ambaye ana cheo. Sababu ya delay nyingi ni huyu bwana anaingilia kati kila proposal za SGC zinapotumwa."

"Mmmm" aliitikia Ed huku mistari ikionekana kwenye paji la uso wake kuonesha hakupenda alichosikia..

"Lakini si hivyo tu tunaifuatilia nini kinaendelea kati yake na Waziri. Kesho watakutana. Tutakujulisha zaidi".

"Ok" aliitikia na kukata simu. Sasa alikuwa kafika nyumbani. Baada ya kuegesha gari aliingia ndani na kukutana na Coletha ambaye alikaa mezani tayari kupata chakula.

"Big Bro umewahi, karibu ufikie hapa" Coletha alimkaribisha kaka yake.

"Usijali sisy, niko vizuri, endelea tu tafadhali." Ed alimjibu na kuanza kuelekea kwenye ngazi zinazoelekea chumbani kwake.