webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

BEAUTIFUL

"Rian" Aretha akamuita

"Ahmmm" Edrian akaitika.

"Asante kwa kila ulichofanya na unachoendelea kufanya. Siwezi kuzuia furaha ninayoisikia ndani yangu kuona unajali ndoto yangu. Nakuahidi kufanya kila niwezalo kufikia uwezo wa kujisimamia mwenyewe."

Aretha akajieleza kwa ukunjufu wa moyo, huku akijaribu kuyazuia machozi yaliyoanza kujaa kwenye macho yake.

Edrian akatabasamu mkono wake mmoja ukabaki kwenye usukani wa gari huku ule mwingine ukigusa shavu la Aretha ambaye taratibu alilaza uso wake pale.

"Asante Rian"

Hisia za mapenzi zikatawala kati yao, Edrian akijaribu kujizuia kutaka kumkumbatia Aretha.

"Oooh sorry, nimesahau unaendesha" Aretha akashtuka

"Ahmmm" akaitika Edrian kana kwamba aliitwa huku akishukuru Aretha kumwachia, joto la mwili wake lilipanda. Uhitaji wa mwili wake ulikuwa katika vita kutii mamlaka ya utashi wake. Akarudisha mkono kwenye usukani na tayari walikuwa wamekaribia mahali ambapo onesho la Beruya lingefanyika.

Ukumbi wa 'Southern Pole' ulikuwa ndani ya jengo la ghorofa saba. Kwa Edrian kushiriki katika maonesho kama haya hakukuwa sehemu ya ratiba zake lakini alipenda sana sanaa ya uchoraji. Hivyo kumleta kwake Aretha hapa ilikuwa kupata fursa ya kuona maandalizi yanakuwaje na kwa namna gani SGC ingenufaika na ushiriki wake.

"Retha" Edrian alimuita baada ya kuwa ameegesha gari.

Aretha akageuka kumwangalia usoni, "eehmm"

"Can I kiss you please" Edrian akaongea kwa sauti ya kumsihi sana Aretha kwa kuwa alijua unaweza kuwa si wakati mzuri.

Macho ya Aretha yalihama kwa aibu lakini kitu ambacho Edrian alikiomba kilikuwa ni kile alitamani kukifanya muda mfupi uliopita. Akatikisa kichwa kukubali.

Edrian akamshika kidevu Aretha kumfanya amwangalie machoni.

"Retha, I want to see the best of you" akasema kwa sauti ya chini huku akiinama taratibu kuelekea kwenye mdomo wa Aretha. Akampa busu jepesi kwenye shavu lake. Akafanya hivyo kwenye shavu la pili, kisha kwenye paji la uso, akarudi kwenye mdomo. Akaibusu midomo ya Aretha taratibu hadi taratibu ilipogeuka kuwa busu zito. Aretha akampa ushirikiano wa kutosha na kwa pamoja wakajikuta katika mahaba mazito hadi Edrian alivyoachia kupeana nafasi ya kupumua.

Aretha akageuka upande wa pili, akajaribu kujiweka vyema maana nywele zilikuwa zimevurugika kidogo!

"Naomba nikuweke vizuri princess. Am sorry" Edrian akamuomba Aretha baada ya kuona akihangaika..

"Aaah" Aretha akashtuka lakini alikuwa amechelewa maana Edrian alishatoa kitana kwenye sehemu ya kuwekea simu na kutaka kumchana.

"Rian naweza kujiwe_" akajaribu kumuomba ampe kitana lakini Edrian hakumpa akaendelea kuuelekeza mkono kwenye kichwa chake ili apate kumchana.

"Please" Edrian akamwangalia na macho kama mtoto anayeomba kitu

Aretha akatulia kumruhusu amuweke vizuri japo kwa aibu nyingi. Alipomaliza akatabasamu

"You are beautiful Retha" akarudisha kitana.

"Eehm..asante"

Wakashuka na kuelekea sehemu ya kuingilia ambapo kulikuwa na eneo la mapokezi. Edrian alihakikisha hamuachi Aretha hata kwa hatua moja. Watu wachache waliokuwepo pale chini waliwaangalia huku baadhi yao wakimsalimu baada ya kumfahamu.

Baada ya kupewa maelekezo waliingia kwenye lifti iliyowapeleka mpaka ghorofa ya sita. Wakaelekea mlango wa kuingilia ukumbini hapo. Kulikuwa na matengenezo yaliyoendelea ukumbini pale kama sehemu ya maandalizi.

"Oooh Mr Simunge, Aretha karibuni" sauti ya Beruya iliwaondoa kwenye fikira zilizokuwa zikipita kwenye kichwa cha kila mmoja.

"Karibuni sana" akanyoosha mkono kumsalimia Edrian na kisha akaelekeza kwa Aretha.

"Meneja wangu amekuja ofisini kwako" Beruya akamwambia Edrian huku akiwaelekeza mahali kulikuwa na viti na meza

"Atahudumiwa vyema bila shaka" akajibu Edrian

Wakaketi, wakati huo Beruya akawakaribisha vinywaji vilivyokuwa kwenye kijokofu kidogo kilichokuwa karibu na meza.

"Aretha tafadhali jione kuwa uko mahali pako ulipopazoe" akamwambia baada ya kumuona Aretha akiwa na wasi wasi usoni..

"Aaah asante sana Beruya, niko vizuri" Aretha akamjibu

"Naona matengenezo yanaendelea" Edrian akamwambia Beruya ambaye alikubali na kumpa maelezo.