webnovel

Tafadhali, Nipende(Please, Love me)

Kuwa na kila kitu kizuri kwenye maisha haimaanishi kuwa una furaha. Ed ni kijana mwenye mafanikio makubwa  akiwa na umri mdogo. Wengi waliyatamani maisha yake, na kwa sababu hiyo alikuwa ni role model kwa vijana wengi wenye ndoto ya kufanikiwa. Akiwa kijana mdogo alijiwekea malengo ya kutoyaleta mapenzi kabla ya wakati wake. Alitumia muda mwingi kuweka imara msingi wa biashara zilizomilikiwa na Simunge Group of Companies. Aliogopa kuyapa nafasi mapenzi wakati alikuwa na mengi ya kufanya. Hakutaka kuona akishindwa pande mbili LAKINI baada ya muda kwenda na kwa msisitizo kutoka kwa mama yake, Ed anaamua kujitosa kupenda, lakini hakujua ni kwa namna gani mapenzi yanaweza kukuchezesha kamari na ukabaki njia panda. Bila kujua yeye anapanga na wapo wanaopanga katika mipango yake. Martinez Kussah mfalme wa kupindua meza na kuyapanga matokeo anayotaka. Kabla Ed hajatweka ndoano yake kilindini kupata samaki, Martinez anamrushia samaki, Joselyn Martinez. Ajali ya kukutana uwanja wa ndege, inapelekea kuingia ndege moja. Haikuishia hapo, viti vinavyoambatana Business Class na mwisho hoteli moja. Coincidence? La hasha Mwanaume mmoja nyuma ya haya anahakikisha jambo lake lazima lifanikiwe. Baada ya Ed kufahamiana na Joselyn anaanza  taratibu kuyaonja mahusiano ya mapenzi, lakini haachi misimamo yake, na anaiweka wazi kwa huyu mpenzi wake. Hatojihusisha nae kimwili hadi atakapomtangaza kuwa mke wake, bila kujua kuwa Joselyn ni mlamba asali asiyeweza kuliacha sega. Ed anakuta amevunja kanuni ya kwanza, na kumbe nyuma ya haya mkono wa Joselyn ulihusika. Na kwa sababu he is a man of his word analazimika kuendelea na safari hii ya mapenzi. Wiki tatu kabla ya kumvalisha pete, anakutana na simple girl Aretha, mchoraji. Picha ya binti huyu inakamata ubongo wa Ed, anaanza kuona kiza katika maamuzi yake. Anapojaribu kuwa karibu naye, kumbe kuna makundi mawili ya watu yanamsogelea huyu binti. Wale wanaotaka kumtumia kubadilisha maamuzi ya Ed na wengine wanataka kumuondoa mbali na Ed. Sasa maisha ya Aretha yanakuwa hatarini zaidi ikiwa yuko on the badside ya Martinez.  Kabla ya haya makundi kupenyeza agenda zao, kundi la tatu lililo hatari zaidi linaibuka. Ed yuko njia panda ya kupambania moyo wake au misimamo yake, biashara au maisha yake. Amuokoe Aretha au aendelee na Joselyn. Let's wait as chapters unveil the desires of Edrian heart.

Evelyne_Buc · Hiện thực
Không đủ số lượng người đọc
245 Chs

BAHASHA NYEUPE

Lyn hakusema chochote akatoa bahasha nyeupe katika mkoba wake, ilifungwa vyema ikionesha haikuwa ukafunguliwa. Akanyoosha mkono kumkabidhi ile bahasha Ed lakini akasita akarudisha na kumuuliza,

"Babe, bado una msimamo ule ule wa kumpa Aretha nafasi yangu?"

Ed akamwangalia kwa hasira, "Muda wako unakaribia kuisha Lyn, nakusikiliza kisha niache nifanye kazi. Unajua masharti yangu linapokuja suala la kazi"

"Ooooh sijasahau babe, ninakumbuka sababu dunia inajua mimi ni mpenzi wako" Alipomaliza kusema akasukuma bahasha kwa Ed akaegama kwenye kiti..

Ed akamwangalia kumuuliza afanye nini na ile bahasha,

"Fungua babe" Lyn akamuonesha

Ed akachukua ile bahasha na kufungua, akatoa picha ambazo aliziangalia kwa utulivu. Kabla ya kuzimaliza akainua macho na kumwangalia Lyn akamuuliza, "Hizi nazo unazituma mtandaoni?"

"Hahahhaha hapana babe, hizi zitaenda kwa mtu anayetaka kukuiba mikononi, nataka ajue mimi na wewe tumekuwa na safari kwa muda mrefu!"

"Mmmmmm" Ed akaguna

"Ooooooh usikasirike babe, mimi na wewe tunapendana ila nadhani ulipomshika mkono siku ile kwenye show alikuroga"

Mikunjo ilionekana usoni kwa Ed, akamwangalia Lyn kiasi cha kumchoma kwa ukali wa macho yake.

"Babe, mbona unanikasirikia bure! Yeye ndie katuingilia, hizo picha ni ushahidi tu ya kuwa tuko zaidi ya atuonavyo"

Ed akarudisha macho kwenye picha zile, akaziangalia tena. Zilikuwa ni picha zilizoonesha sehemu tofauti walizokuwa pamoja. Lakini chache zilimuonesha akiwa amelala kitandani na Lyn wakiwa wamekumbatiana.

"Okay kama unataka sana..ah Retha azione hizi picha nitakusaidia umfikishie" Ed akasema wakati akizirudisha picha kwenye bahasha na kumrudishia Lyn.

Lyn akabaki akimshangaa kabla ya kucheka kicheko kizito na kuinuka kisha akainama kumuelekea Ed usoni, "Babe najua hautaki ila hatua yoyote ya kuendelea na huyu binti ni gharama ya maisha yako"

"Lyn, unanipotezea muda wangu..nina vitu muhimu vya kufanya kuliko hizi kelele zako. Naomba uondoke" Ed alipomaliza kusema akainuka na kuelekea mlangoni, akamfungulia mlango Lyn

"Hehhehe Ed babe we love each other. Wewe umekusudiwa kuwa wangu." Akachukua mkoba akaelekea aliposimama Ed..

"Umeacha bahasha yako Lyn" Ed akamwambia

"No babe, kaa nayo hiyo na mpatie kama ulivyosema. Nitathibitisha kama imemfikia"

Akamsogelea na kutaka kumbusu, Ed akamzuia kwa mkono wake ambao haukuwa umeshika mlango...

"Tsk. .tsk. .tsk babe I miss you" Lyn akamshika bega na kuondoka..

Ed akaachia mlango uliojifunga taratibu. Akashusha pumzi akarudi kuketi, na kuichukua ile bahasha. Akatafakari ikiwa Lyn atatuma kweli zile picha kwa Aretha inawezekana zikampa mashaka binti yule.

Akaangalia simu yake, muda ulikuwa bado kama dakika arobaini kwa Aretha kuwa ametoka darasani. Akaandika ujumbe mfupi wa simu,

"Retha darlin ukimaliza kipindi nitakuwa karibu na maeneo ya chuo. Usile chakula cha mchana. Tutakula wote. Love you princess."

Akachukua ile bahasha akaitumbukiza kwenye moja ya droo zilizokuwa kwenye meza yake. Akachukua chupa ya maji na kunywa, alipoishusha akacheka sana,

"Mapenzi kumbe huwa yanalazimishwa ha ha ha"

Tik. .tik

Ujumbe ukaingia kwenye simu yake. Akaangalia, "Okay Rian. I love you too" ulikuwa ni ujumbe kutoka Aretha.

Nuru ilionekana usoni kwa Ed baada ya kusoma ujumbe ule. Akaweka simu pembeni na kuinua simu ya mezani

"Allan tunaweza kuendelea na kilichobaki nina dakika chache nitakuwa natoka"

Akarudisha simu mezani huku akiwasubiri Allan na Loy aweze kumaliza alichoanza kueleza kwao. Moyoni alikusudia kuonana na Aretha kwa kuwa alikumbuka kuwa hakuwa amemwambia vile Lyn alimuwekea dawa kwenye kinywaji chake.

"Nahitaji kumwambia mapema, huyu mwanamke ni mgonjwa kweli aweza vuruga mambo zaidi ya ninavyoweza kufikiri" Akawaza Ed.

Mpango ukagongwa. Allan na Loy wakaingia na kuketi tayari kuendelea na mazungumzo waliyoanza na bosi Edrian Simunge.

"Samahani sana kwa muingiliano uliotokea, naamini hautajirudia tena..naomba tuendelee" Ed aliomba radhi kwa Allan na Loy kwa kuwa alijua kama kiongozi lazima akubali kuwa alifanya makosa kwa kuwa Lyn hakuwa mfanyakazi wa SM.