webnovel

CHAPTER 5

Kutokana na lile tukio la kukutana na Angel, ndugu yetu Manuel kumbe alikua akilitizama kwa makini sana, aliniuliza ili apate ubuyu, nikampa story kuhusu mimi na Angel. Manuel akanambia uyo dada the way nimemwona ni anakutaka, cha kukushauri achana naye kabisa,

EX's are toxic my brother especially in a relationships, mara 100 utembee na mtu mwingine lakini sio Ex.

"Vipi ulimpa namba yako" Manuel aliuliza, nikamwambia hapana, akanambia bro you're genius.

Niliamua kufuta namba ya Angel na sikutaka kuweka ukaribu naye kabisa, mtu aliyekuacha unapata wapi nguvu ya kumtafuta??, bora ningemwacha mimi hapo sawa, nilikua nikijiambia moyoni.

Wakati bado niko parking pale ghafla simu ikaanxa kuita, kucheki ni Maggy nikapokea alikua anasisitiza na kukumbushia suala letu tulilokubaliana, nikamwakikishia hakuna jambo litakalo haribika.

Kumbuka hapo nina wateja wawili na wote wanaelelea Posta, nikajiambia hakuna shida nitawapanga mapema kila mtu ajue atakua na mwenzie.

*****

Nikawasili pale kwa wakwe nikamkuta Mama mkwe, dada zake, wadogo zake, tukasalimiana, akanikaribisha ndani. Nikamsalimia mtoto, ukweli hakuna raha ambayo wanaume huwa tunapata kama ukiwa na mtoto ambaye mnafanana, kuna kafeeling huwa tunakapata sana (Nikimwangalia Junior na mimi ni copyright). Sikukaa sana pale maana mimi ni mtu ambaye huwa sipendelei kwenda mara kwa mara ukweni au kukaa sana.

Nikaaga pale, mama J tulikua tumeongozana mpaka kwenye gari, nikampa cash 300k hii ni ile pesa ya Manuel, baada ya kununua mazaga hio ndo ilibaki, nikaona nimpe mama yake. Nikamwambia pesa ilikotoka, maana nilijua wazungu huwa hawasahau na wanapenda uaminifu sana, ipo siku atauliza tu.

Baada ya pale nikasema acha nirudi home nikalale niweke mambo sawa kwaajili ya kesho.

Nikampigia simu Maggy na Mama ( tumwite mama wawili(2)) nikawapa mpango mzima kuhusu mkataba na kila mmoja nikamtumia soft copy. Sasa pale home nilikua na jamaa yangu mwanasheria nikampa hardcopy anipigie mhuri.

*****

Ilikua jumatatu njema kabisa nikaamka mapema sana, nikajiandaa vizuri kabisa nikapulizia na unyunyu wangu huyo nikawasha chombo kuingia mzigoni, ilikua 06:25 asubuhi nilikua tayari kwa mama wawili. Mimi nilikua nakaa mbezi beach shule so haikua mbali lakini huyu mama sikumwambia nakokaa.

Nimefika pale nikampigia uzuri na yeye alikua tayari na mtoto wake, Nikamsalimia, akanambia uko sharp sana. Nikamdrop mwanaye pale shuleni, nikamwambia kuna mtu pia tunamchukua pale Alpha uzuri Maggy alikua yuko pale barabarani nikamchukua akaja akaa mbele, Mama wawili siku hiyo alikaa nyuma na mwanae.

Nikawadrop pale Posta, nilianza na Mama wawili pale Azikiwe nikampa mkataba wake nikamwambia utausoma afu utajaza, nikasogea mpaka pale Golden nikamdrop Maggy naye nikampa mkataba akanambia ntakucheki kaka, nikamwambia sawa bossy wangu.

Kukamilika kwa deal la Maggy & Mama wawili nikawa na uhakika wa kuingiza 484,000/= kwa mwezi, nikajisemea mwanzo mzuri.

Nikapark gari yangu palepale ambapo nilimiti na Maggy nikiwa nasubiri request, saa yangu ilikua inaonesha ni saa 2 mbili tayari na madakika yamekata. Nilikua nimeshuka kwenye gari baada ya kumwona dada wa TARURA na kimashine chake akisogea upande wa gari yangu, nikawa namzingua , "Dada mapema hivi unataka kuchora subiri kidogo kukuche" kwanza Kaka gari yako inadaiwa 5,000 inabdi ulipe.

Hawa dada wa TARURA walikua wananikera sana yaani usipark gari pembeni chap kashakuja kuchora, sasa mimi nilikuaga nazinguana nao sana.

Muda uleule nikapata request ilikua location inaonesha customer yuko pale Serena Hotel, akanitext via App, gari yako ina AC? Nikamjibu ndiyo, akanambia njoo chap hapa Serena. Kufika pale namwona mfanyakazi wa pale anatoka, ndo yeye alikuwa karequest akaniuliza wewe ndo INSIDER?, nikamwambia ndo mimi, Ok subir anakuja, Park vizuri na wengine waweze kupita.

Ndani ya dakika 5 akafika mzee, tuseme ni mzee kijana, "kijana wangu hujambo?"…sijambo mzee pole na majukumu "salama sana" si umeona tunakwenda Ununio, nikamwambia sawa mzee wangu.

Nikampeleka mpaka Ununio nikamshusha nikamsaidia kutoa bag lake, sasa kijana itabid unipe namba yako ntakupigia, sawa mzee haina shida huyo nikaondoka.

Nikadrive mpaka pale Ununio shuleni nilikua najua pale lazima nikutane na wahuni na pale huwa ndo kijiwe cha Uber. Nikawa nimechili pale huku nikicheza draft na masela, kila nilikokua natega au kila kijiwe bhasi nilikua najitahidi sana niwe na ukaribu na watu wa eneo hilo.

Nikacheki whatsapp chats nikakuta Manuel kanitext "Hey bro! Good morning, we arrived safely, I'll call you later",.

Hii siku biashara kwangu haikuniendea vizuri nakumbuka nilikaa pale mpaka saa 6 mchana ndo nikaja kupata request mteja alikua anakwenda mwenge.

*********

Kazi ya kuwachukua akina Maggy ilikua ikiendelea vizuri na wote walikua washarudisha mikataba yangu ile jumanne wakati mama anarudisha mkataba alinambia wewe kaka upo serious asee, mpaka umegonga mhuri wa mwanasheria nimekuvulia kofia…" nikamwambia mama hii ni ofisi lazima niwe serious kama nimeandaa mkataba wa kijinga ukanikimbia itakuaje??". Upande wa Maggy yeye alifurahi jinsi navyofanya kazi serious, Maggy ni dada ambaye nilikua nikimwona yuko serious sana na maisha.

Licha ya kuwapa mkataba tu pia niliomba copy za vitambulisho vyao, na kwenye mkataba wangu vipengele muhimu nilivyoweka ni pamoja na, mkataba ulikua wa siku 22 kwa mwezi toa jumamosi na jumapili

*****

Hii tulikua tumeanza week ya Christmas ukweli ni kwamba kipindi hiki kazi zilikua nyingi sana na pesa ilikua inaonekana, sasa nakumbuka kuna tukio lilinitokea siwezi kulisahau kwakweli.

Ilikua ni jumatano usiku nilikua nimemchukua dada mmoja hivi kutoka pale Slipway Masaki ilikua ni saa 3 usiku alikua anaelekea Sinza, sasa wakati nimefika anapokaa nika end trip na nauli ilikuja 10,000 tu. Dada akanambia kaka mimi sina hela tumegombana na boyfriend wangu hajanipa hela, nikamwambia sasa mbona hukusema mapema kama huna?, umenyamaza kimya mpaka tunafika hapa.

Nikamwambia dada wewe sema leo biashara imekua ngumu ila usianze kudanganya hapa mimi mzoefu naelewa, nikamwambia sasa naipataje hela yangu?, nikupeleke lodge au humuhumu kwenye gari??…. Kwanza lodge mbali ntapoteza pesa zangu namalizana na wewe hapahapa, mvua nguo chap (huku nimemkazia macho)…. Eeh dada si kweli akaanza kufungua kifungo cha pant yake. Dada stop! mimi sio kama wanaume wengine hii kwangu ni ofisi naomba nitumie hiyo pesa kwenye nmba yangu kama utanidhulumu ni wewe.

Kaka ahsante ntakutumia una roho nzuri sana, nisave nani jina lako nikamwambia wewe utavyoona sawa, huyo nikasepa. Kesho yake dada kweli akatuma pesa, akanipigia simu kaka nimetuma, nikamwambia hapo umetisha sasa tuongee biashara wewe nakupataje?? anytime wewe ukiwa tayari , nikajisemea kwa hali hii madereva wa Uber tutakufa kwa ngoma, hata maendeleo tutasahau.

*******

Ilikua imeshakata week yule mzee ambaye nilimchukua pale serena hotel kumpeleka Ununio alinipigia simu, ilikua ni 24/12 usiku,

….

Mzee: kijana naomba kesho uje pale nyumbani, si unapakumbuka??,

Mimi: ndio mzee napakumbuka,

Mzee: bhasi kesho uje saa 3 asubuhi, tutakwenda Mbweni na Kigamboni, gharama zako zikoje?

Mimi: Mzee inategemea na root zako ila gharama zangu kwa siku kutoka asubuhi- Jion 18:00 ni 150,000/= na kuendelea ila maongezi yapo.

Mzee: kijana gharama zako ziko juu sana, punguza kidogo

Mimi: mzee kipindi hiki cha sikukuu rate za nauli zimeongezeka sana na pia kumbuka nakua na wewe siku nzima, top kabisa 120,000/=

Mzee: Haina shida bhasi kesho mapema uwai kijana, nakusisitiza

Mimi: haina shida mzee wangu,

Ilikua ni Christmas afu sasa ilikua ni jumamosi sasa hii ni siku ambayo nilikua na miadi na Mzee. Nilifika mapema sana pale Ununio kama tulivyokubaliana, mlinzi akanifungulia geti nikawa namsubiri pale parking. Mzee parking yake ilikua na VX na BMW X5, nikasema Kuna watu wana hela asee, kwanza nyumba yenyewe ni ya kibabe.

Baada ya nusu saa mzee akaja pale na bag dogo la kuvuta, nikaliweka kwenye buti, safari yetu ilikua inaanzia kwenda Mbweni. Mzee mbweni alikua anakagua nyumba yake pale, tulikaa kama saa 2 hivi tukatoka kuelekekea Kigamboni.

Saa 7 tulikua kigamboni sikumbuki panaitwaje ila ni mbele ya Pweza beach, kufika pale ilikua ni apartment ya nyumba 3 ndani. Mzee akanambia Kigamboni tunakwenda kwa mchepuko wake atakaa mpaka jioni afu tutarudi Ununio ana wageni badae.

Baada ya kufika akatoka dada pale kumpokea mzee (mchepuko wake), baada ya kuuchunguza kwa makini mchepuko wa Mzee, nikajisemea Mzee anajua kuchagua. Mzee akanipa 30k, akanambia niende nakojua mimi ila 17:00 ontime niwe pale, kumchukua, nikasema acha niende Pweza Beach nikapoteze muda tu.

Mnajua hizi kazi za Uber sometimes ni za ki**nge sana, naonaga hazinaga utofauti na utumwa, ndomana mimi nilikua sibembelezi sana customer wa kufanya naye kazi kama hafikii rate zangu namwacha. Nilikua najiamini course nilikua napata kazi nyingi so sikua na shida na tamaa za kijinga.

Nikachili pale Pweza beach nikasema simpigii Mzee simu mpaka anicheki mwenyewe, kucheki muda ilikua saa 11 na madakika kadhaa tayari hapo mzee hajanicheki, nikasema acha nisubiri mpaka ifike 17:30 nimpandie hewan, japo alisisitiza sana muda huo niwe pale.

Muda ukawa umefika 17:30 nikaona bado kimya nikasema nimpigie au niache?? Lakini nikawa najiuliza mwenyewe kama nayeye anasubiri nimpigie??. Nikampigia simu lakini cha ajabu naambiwa namba haipatikani, nikarudia tena namba haipatikani, nikaamua kwenda tu kumfuata.

Nafika pale lakini gate likikua limefungwa na hakuna mtu around wa kunifungulia, nikaanza kujiuliza kwamba mzee kapelekewa moto sana?, nikashuka kwa gari, nikagonga geti lakini hollaa! hakuna anayekuja kufungua.

Hii siku ilikua jumamosi afu Christmas demand ya usafiri ilikua juu sana na nauli pia zilikua juu sana licha ya kumaliza kazi ya mzee nilitamani sana niingie barabarani niendelee na mzigo. Dullah before alikua kanicheki whatsapp afu kanitumia ubao wake, yaani mpaka sa10 mchana alikua kashakusanya 120k, niliingiwa na roho ya wivu.

"Kipindi kama hichi cha sikukuu Uber huwa tunaringa sana sehemu ambayo haina manufaa huwa hatuendi maana request zinakua nyingi sana."

Wakati nikiendelea kutafakari pale nje getini, Mama J akaanza kunipigia simu, nikakumbuka aliniambia niende kwao kuna chakula cha pamoja kama mimi moja ya familia natakiwa niende na baba yake (baba mkwe) atakuwepo, "nilikumbaliaga kuwa nitakwenda". Nikapokea simu yake akanambia mbona mpaka sasa hujaja?, sikutaka ugomvi nikamwambia ntakuja badae wewe usiwe na wasiwasi.

******

Ilikua ishafika 12 na madakika tayari ndo kuna dada alikua anatoka, nikamwuliza kama ana mazoea na yule mchepuko wa mzee, akanambia sina. Nikaingiza gari ndani ikabidi nigonge mlango kama dk 3 dada akatoka, nikamwambia mzee hapatikani na alinambia 17:00 niwe hapa ontime. Dada akanambia mzee kalala toka saa 10, nikajikuta nataka kucheka, nikamwambia dada amwamshe tuondoke maana tushachelewa tayari.

Baada ya dk 15 mzee alikua tayari katoka kwaajili ya safari, nikamwambia mzee nilikua nasubiri unipigie lakini nikaona kimya, kukupigia hupatikani akanmbia bhs dada alizima simu yangu, kucheki kweli simu ilikua imezimwa. Mzee akaniomba tuondoke chap maana saa 1 anawageni muda huo ilikua sa1 kasoro tayari.

Tukatoka pale Kigamboni lakini barabarani kulikuwa na foleni sana tukajikuta tunafika Ununio saa 3 kasoro, mzee akanipa pesa zangu akanambia atakuwa ananicheki, nikamwambia haina shida.

Muda huo nilikua nishawasha App yangu muda sana nasubiri request, haikuchukua muda niakapata request ya kwenda Airpot, ile nime accept tu, ni kama dada alikua anashida sana ya usafiri palepale akapiga simu, "kaka naona haupo mbali na mimi,please njoo haraka nachelewa". Ofcourse alikua mtaa wa pili unaofuata, nikamkuta yuko nje getini tayari, ile nashuka dada anambia yaani kaka kama bahati leo usafiri wa shida sana, nikamwambia dada hujui leo ni sikukuu??

Tukatoka hapo chap kuelekea JNIA so dada alikua na haraka sana, alikua anaomba nikimbize gari, ni kwamba dada alikua anaondoka na ndege ya 22:30 afu alikua anatakiwa kuchek in 20:30 na muda huo tunaondoka ilikua ni 21:45. Nikamwambia dada mimi huwa siendeshagi zaidi ya 60km/hr kwa mjini humu, kutokana na kusema Uber zilikua za shida na mimi natambua hili nitakuwaisha ili uwai ndege, dada akashukuru.

Sikutaka kutumia Bagamoyo road maana nilijua kutakua na foleni tu watu wanakwenda mjini kula bata. Nilikua nazijua shortcuts baadhi ya njia so nilipita chini kwa chini nikaja kutokea Ununio, hii barabara niliyopita kipindi kile ilikua inatengenezwa lakni sahivi ina lami. Nikatembea chinichini kwa chini kufika kunduchi nikaingia na barabara inayopita cota za Police hao tukatokea kwa "Mwamnyange" nikaunga na Mwaikibaki road, hao Mikocheni nikaingia na barabara ya ubalozini ghafla tunajikuta tushafika namanga huyo nikaunga na "Alli Hassan Road". Dada muda wote macho kwenye simu akiangalia muda huku aniangalia mimi starring navyopambana na Road.

Ilinichukua dk 40 kuingia JNIA terminal 3, dada alifurahi sana hakuamini kama angewai lakni bado alikua na wasiwasi kama kachelewa.

Vipi unaondoka na ndege gani?, KLM nikamwambia usiwe na wasiwasi umewai sana, nauli ilikuja 32,000 dada akanipa 40,000 nikataka mpa change akanambia keep it. Nikamsindikiza dada mpaka anaingia ndani mimi nikakaa pale nje kwenye vile vibaraza, " Sheria za Airpot hauruhusiwi kukaa ndani ya gari", haikuchukua dk 5 dada akanipigia simu kaka ahsante nimefanikiwa, namba yako nimesave ntakucheki nikirudi, nikamwambia sawa, safari njema.

Wakati nimekaa pale nje nikisubiri request nilikua napiga story na moja ya mlinzi wa pale, nilikua najaribu kila nakokwenda niwe na watu naowajua hata kama kuna jambo au msalaa nakuwa ba backup. Nilikua namuuliza jamaa kwanini Uber tunazinguliwa sana mle ndani, jamaa akanifungukia akanambia zile gari/tax za Airpot ni mradi wao na pia ni gari za wakubwa humu ndani, uwepo wenu nyie Uber umepelekea biashara zao kuwa mbaya. Hapo ndo nikajua kumbe ni biashara za wakubwa mle ndani ndomana kuna vita na madereva wa Uber.

Wakati story zikiendelea na jamaa nikapata request, kuwasiliana na mteja akanambia yuko Airpot pale Puma filling station, nikamwambia mteja mimi niko terminal 3 kutoka hapa si unajua lazima nilipie getin pale akasema hiyo 2,000 mimi ntakupa fanya chap mimi nachelewa.

"Huyu mlinzi alikua mshikaji wangu sana alikua ananipa ratiba za ndege kutua nknk, alikua ni asset kwangu", huko mbele mtaona.

Nikamwaga jamaa tukaexchange number nikampa buku 5 ya soda huyo nikapotea, kufika kwa jamaa pale Puma nikampakia alikua na demu wake, safari yetu ilikua ni kuwapeleka pale Whitesand hotel. Wakati nakaribia Whitesand nikiwa pale Ramada hotel nikapata request juu kwa juu "hii mara nyingi inatokea kama upo karibu na mteja au kama usafiri wa shida", muda uleule customer akapiga simu, dereva njoo hapa "The wave" nikamwambia ASAP.

Nikamdrop jamaa na demu wake nikapitia kumchukua mteja pale "The wave", hao ulekeo ulikua ni Tips Mikocheni, Pale sikukaa hata nikapata mteja alikua anakwenda Samaki samaki, Masaki. Mpaka muda huo ilikua ishafika Saa 7 usiku na madakika kadhaa, nikasema acha nitafute sehem nipark na pia nipunguze mafuta yangu ya mwilini.

Ile mitaa ilikua imejaaa sana magari sana yaani kulikua kumefurika kumbuka ilikua ni Christmas, kuanzia kule Elements yaani mpaka unakuja Samaki samaki, kumefura hatari, parking za shida afu Masai wakiona IST wanajuaga ni Uber wanazinguaga hatari .

"Masai huwa hawatupendi kwasababu huwa hatuwapi hela, mimi kutokana na gari yangu nilikua natumia vibao vya njano, nilikua hawanisumbui kabisa, kama ukipark usiposhuka anakugongea anauliza wewe ni Uber au laah"

Nikasema ngoja nisogee mpaka kule chin kama unakwenda Village supermarket, sasa nikaamua kupark pale kwenye corner inayokwenda UN pale kuna ka uwazi mitaa , Ile napark gari tu aisee si nikavamiwa na wale "DADA POA" sikujua kama ni chimbo lao lile, ila walikua mapini hatari.

Sikupenda ule usumbufu nikaamua kutoka pale wakaanza kusonya huku wananitukana, nikasema leo nimevamia mtumbwi wa vibwengo.

Nikapata request pale Samaki samaki nikamfuata mteja alikua ni dada lina mahips hatari afu lizuri, akanambia kaka mimi naelekea bwawani ila map iko sawa, wewe twende. "Bwawani ni mtaa ambao unaingilia pale Kinondoni kanisani sijui kwa Selebonge ni maarufu sana kwa mapishi, sasa unakunjia corner pale au njia nyingine unaingilia pale mbele baada ya jengo la Vodacom kuna mataa pale, barabara za kule ni za nzege".

Nikamsusha yule dada pale, kucheki muda saa 9 na madakika yake nikasema ngoja nikatege pale Tips then nikalale, kutoka pale Bwawani mpaka Tips sio mbali. Nikasogea pale Tips napo palikua pamejaa hatari si unajua sikukuu imeangukia jumamosi kila mtu katoka out.

Mida kama ya sa10 ilikua imefika nikapata request ya kwenda Maison club, hii club ipo karibu na Sea cliff mitaa ileile. Wakati nimemdrop pale mteja nikasema acha niset destination ya mbezi beach mimi pia nikalale ili kesho niendelee na mzigo mapema. Kipindi cha sikukuu ndo kipindi ambacho Uber wanaingiza sana Pesa ni kipindi cha kuwa serious na kazi.

Palepale Maison nikapata request na mteja alikua anakwenda Mbezi beach kwa Zena, nikafurahi sana maana destination mpaka uipate ni bahati sana. Huyu alikua ni demu ana uchotara flani hivi aisee ni pini hatari akaingia akakaa mbele, akakilaza kiti ili alale vizuri mimi namwangalia tu, akanambia kaka fata ramani "alitoa sauti ya kudeka". Ilikua ni pini balaa, kama wewe ni mwanaume rijali lazima utingishike, kwanza dem toka anaingia kwenye gari wahuni walikua wanamtolea macho balaa.

Alivyonambia fata ramani mimi sikua na swali tena kwani ramani ilikua inanionesha uelekeo ni mbezi beach, tukaanza safari pale nilipita ile barabara inayokuja tokea pale Tanesco Mikocheni, tukaunga wakati tunafika pale round about ya Kawe, dizaini kama dada akaanza mitego, mara atanue miguu, kama mtu ambaye anahangaika hivi.

Tulivyofika pale Rainbow kwa mbele si kuna filling station ya GBP, nikazama pale ili kuweka wese, nikashuka pale ili nipate na kaupepo kidogo huku jamaa akiweka mafuta, so ile naingia kwenye gari nakuta kile kigauni kimepanda mpaka saizi ya kiuno yaani naona kila kitu live, naiona chupi hii hapa live, paja hilo huku kwangu frequency zishachange muda, afu namuda sijapata ile kitu si unajua wife alikua hayupo.

Kwa muda ule nilikua sielew nini cha kufanya maana tamaa ilinijia haraka sana ya kumla yule dada, nikamgusa chupi pale katikati nikaona dada anaanza kuhangaika, huku akitoa ushirikiano, nikasema leo Mbuzi kafia kwa Muuza soup, naiachaje pisi kali kama hii….