webnovel

HALWA HALWA

Umaskini waweza ukakupoza. mapenzi watu hawayadhamini kisa na maana moja kazaliwa familia ya kimaskini na mwenzake ya utajiri. Je Sophia ataweza kujimudu na kufunga ndoa na Lui. Je Lui yuko tayari kuachwa bila chochoti kisa mapenzi.... ....................... I am doubtful if I can get readers so I will only publish for chapters if I get people to criticize the book then I will keep on writing.

nizah · perkotaan
Peringkat tidak cukup
1 Chs

Umaskini

Sophy! Sophy!

Jamani wewe Amina mbona fujo kelele hadi mtu akiwa ndani anasikia fujo zako. Haya una nini?

Sophy nilipokuwa njiani naja pale kichochoroni pa mama ntilie nimekutana na dadako tausi ela alikuwa apigwa na vijana wawili sijui wamekaa aje aje!

Sophy amatazama Amina na kumshangaa sasa hiyo mimi yanihusu vipi?

Aaa dada wewe huna huruma wala utu nakwambia dadako anapigwa kisha huna hata wasiwasi.

wewe mwenye wasiwasi mbona hukumsaidia. Sophy apandwa na mori na kumfokea Amina.

Wewe mwanamke mbona mbeya hivo fwata yanayo kuhusu yasio kuhusu achanana nayo.

Haya kama huna lingine la kusema naomba utoke nina mambo yamuhimu nataka kufanya.

Sophy hakupoteza muda akafunga mlango wake bila ya kumpisha Amina ndani.

Amina akiwa nje akashangaa shoga yake leo ana nini mbona aonekana mwenye majozi. Amina akatoa Simu yake na kumpigia mpenziye Akram.

Simu ikaita mara kadhaa kabla Akram kuipokea. Hello Amina Akram akamsalimu mpenziye kisha akamuliza mbona wanipigia siwewe umeniaga eti umeenda kwa shoga yako Sophy.

Nimeenda na nimemkuta ela nadhani ana tatizo wajua hajanipokea amenifokea na mwishowe akafunga mlango wake na kuniacha nje nata nashangaa nilichomkosea jamani. Akram waweza kuwa wajua kinacho msumbua Sophy?

Akram akamjibu kwa mapenzi sasa "mpenzi wange mimi nitajuaje mambo ya kike? wewe jaribu kumzungumzisha ujue kinachomsumbua mimi hapo siwezi kukusaidia.

Amina haya basi Habibi baadaye.

Sophy mwanangu njoo unipokee mamake Sophy anaonekana Akija na mzigo.

Aaa Amina wafanya mini mlangoni kweni Shoga yako hayuko ndani.

Amina Shikamoo mama. pole kwa uchovu mama. Ndio nimefika mama nimesha mtarifu Amina kupitia kwa zamu. Aaa basi twende ndani Amina.

Samahani mama naomba nikupokee mzigo wako waonekana mchovu sana.

Asante mwanangu napenda tabia zako Mwanangu Imran nigetamani ampate mke muadilifu kama wewe.

Asante mama.

Amina Anamsaidia mamake Sophy mzigo na wote wanaingia ndani. mamake sophy anaenda moja kwa moja hadi chumbani mwake na kumwacha Amina sebuleni. Jiskia nyumani akina wacha nikajipumzishe ndani.

Sophy wanatoka jikoni akiwa amebeba glasi ya shurbeti. Anapomwona Amina anashtuka na kumgeukia wewe aliyekuruhusu humu ndani ni nani. Nadhani nilikuwa mwazi nilikwambia leo sitaki umbea wako! kisha Tausi yuko wapi siuliniamwia umemwacha njiani watu wakimpiga sasa hukwenda kumsaidia.

Amina anashikwa na hasira Sophy sijui kwa nini leo wanizungumzia hivo kumbuka mimi rafiki yako wa dhati kama nimekukosea niambie wacha kunisimanga hivo.

sophy anamwangalia shoga yake kisha machozi yamdondoka. mwenziwe anamshangaa jamani shoga kunanini? mbona walia

Sophy anamwangalia mweziye kisha anamjibu umaskini mwenzangu wanipoza...

wamanisha nini...

utaelewa siku moja kwa sasa huwezi nielewa.